RASMI: King Kibadeni kocha mpya wa klabu ya Simba SC ya Dar es Salaam . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, May 27, 2013

RASMI: King Kibadeni kocha mpya wa klabu ya Simba SC ya Dar es Salaam .



King Kibadeni. 
Klabu ya Soka ya Simba imefikia Makubaliano na Abdallah Athumani Seif maarufu kama King Kibadeni  kuwa kocha mpya wa klabu hiyo ya Simba ya Dar es Salaam .




Katibu wa Simba SC, Evodius Mtawala sasa anaandaa Mkataba kulingana na makubaliano na Kibadeni aliyekuwa kocha wa Kagera Sugar ya Bukoba msimu uliopita , kisha ataupeleka kwa Kamati ya Utendaji ya klabu ukapitiwe tayari kwa gwiji huyo wa Msimbazi kuusaini Jumatano.




Lakini wakati taratibu za Mkataba zikiendelea, Kibadeni au Chifu Mputa ataanza kazi kesho saa 1:00 asubuhi katika Uwanja wa Kinesi, Urafiki, Dar es Salaam.




Asubuhi ya kesho, Kibadeni atawafanyia usajili wachezaji zaidi ya 40 wakiwemo kutoka nje ya Tanzania ambao wanaomba kusajiliwa na mabingwa hao wa zamani wa Afrika Mashariki na kati na Tanzania Bara.




Baada ya usaili huo, wachezaji ambao watamvutia mfalme huyo wa mabao wa zamani nchini, wataunganishwa na wachezaji waliosajiliwa Simba SC kwa ajili ya msimu ujao kuanza rasmi maandalizi ya msimu mpya Jumatano, Uwanja wa Kinesi.




Mazoezi ya Jumatano yatahusisha wachezaji wote, ambao hawapo katika timu zao za taifa, yaani waliokuwepo kwenye kikosi cha msimu uliopita na wapya waliosajiliwa.




Wachezaji ambao hawatahusika katika programu ya msimu mpya ya Simba SC ni Haruna Moshi ‘Boban’, Amir Maftah, Wilbert Mweta waliomaliza mikataba, Paul Ngalema, Abdallah Juma walioomba kuondoka, Salim Kinje anayetolewa kwa mkopo, Juma Nyosso na Ramadhan Chombo ‘Redondo’, ambao suala lao lipo kwa Kamati ya Utendaji.




Katika benchi la Ufundi, Kibadeni atakuwa anasaidiwa na walimu wawili, Mganda Moses Basena na mzalendo Jamhuri Kihwelo ‘Julio’, wakati Meneja atakuwa Nico Njohole na mtunza vifaa atakuwa Ally Cheche.




Mtihani wa kwanza wa Kibadeni unatarajiwa kuwa nchini Sudan mwishoni mwa mwezi ujao, ambako Simba itacheza Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame pamoja na wapinzani wao wa jadi, Yanga SC.




Simba SC imepangwa Kundi A katika michuano hiyo pamoja na wenyeji El-Mereikh, Elman  ya Somalia na APR ya Rwanda, wakati Yanga ambao ni mabingwa watetezi, wamepangwa Kundi C na Ports ya Djibouti, Express ya Uganda na  Vital 'O'  ya Burundi.




Katika michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Juni 18 hadi Julai 2, mwaka huu mjini Khartoum, Sudan, mabingwa wa Kenya, Tusker wamepangwa Kundi B pamoja na wenyeji wengine, Al-Hilal, Falcons ya Zanzibar, Al Ahly Shandy ya Sudan na Al-Nasir Juba ya Sudan Kusini.




Simba SC itashuka dimbani Juni 21 kufungua dimba na El-Mereikh, wakati mabingwa watetezi, Yanga wataanza kampeni zao za kutetea taji Juni 20 kwa kumenyana na Express na mechi zote zitachezwa Elfashar.



WASIFU WA KING KIBADEN.



19-Alizaliwa mjini Dar es Salaam.


19-Alijiunga na Simba SC akitokea.


1974- Alifunga bao la kwanza katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Hearts Of Oak ya Ghana nchini Ghana katika Robo Fainali ya Kwanza ya Klabu Bingwa Afrika.




1974- Aliiongoza Simba kuwa rekodi ya kuwa klabu ya kwanza na pekee Tanzania kufika Nusu Fainali ya Klabu Bingwa Afrika hadi sasa.




1978- Alifunga mabao matatu peke yake katika ushindi wa 6-0 dhidi ya Yanga SC.




1993- Aliiwezesha Simba SC kufika Fainali ya Kombe la CAF akiwa Kocha, rekodi ambayo haijavunjwa hadi leo ikiwa ni miaka 20 baadaye.




19-Alistaafu Simba SC na kwenda kuwa kocha Majimaji ya Songea.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad