PICHA: Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani wilayani Ngara mkoani Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, May 01, 2013

PICHA: Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani wilayani Ngara mkoani Kagera.


Mokhamed Khalfan akiwa na wanafunzi wake wa Chuo cha  Sekhasa Mining Mjini Ngara.


Walimu wa Shule za Msingi na Sekondari wilayani Ngara mkoani Kagera wakiwa  katika maandamano ya Mei Mosi leo(May 01,2013)kuelekea uwanja wa Posta ya zamani mjini Ngara .


Afisa Elimu Msingi wilayani Ngara Simon Mumbee akiwa na Afisa Elimu Sekondari Julius Nestori wakielekea uwanja wa Posta ya Zamani tayari kwa maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi Duniani.


Afisa Utamaduni na Micheza wilaya ya Ngara Said Salum  akiwa katika kuburudisha maandamano ya May Mosi wakielekea uwanja wa Posta ya Zamani tayari kwa maadhimisho  HAYO ya siku ya Wafanyakazi Duniani..


Wafunzi wa Sekhasa Miningi na Wafanyakazi wa serikali za mitaa wilayani Ngara wakielekea uwanja wa Posta ya Zamani tayari kwa maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi Duniani.

Wanafunzi wa shule ya Msingi Ngara mjini wakiwa katika maandamano ya Mei Mosi 2013.Picha zote na Shabani Nasibu Ndyamukama.




Katika Maadhimisho hayo ya Siku ya Wafanyakazi Duniani pamoja na mambo mengine , Serikali  imeombwa kutatua kero zinazowakabili wafanyakazi nchini  kwa kuboresha mazingira ya kazi sambamba na Mishahara .




Katibu wa TUCTA  wilayani Ngara Bw Vedasto Nsinde amesema serikali haina budi kupandisha mishahara kwa kima cha chini kuwa Shilingi Laki  tatu na elfu 15 kwa mwezi  ili kwenda sambamba na  upandaji wa gharama za Maisha ya sasa.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad