Mchungaji Peter Msigwa. |
Wabunge
waliosimamishwa Aprili 17,2013 ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni ambaye
pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Iringa Mjini,
Mchungaji Peter Msigwa.
Wengine
ni Highness Kiwia (Ilemela), Ezekiel Wenje (Nyamagana), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’
(Mbeya Mjini) na Godbless Lema (Arusha Mjini).
Jana
asubuhi Mchungaji Msigwa alikuwa miongoni mwa wabunge waliowahi kuingia mapema
ndani ya Ukumbi wa Bunge na kufuatiwa na Lissu muda mfupi baada ya kikao
kuanza.
Ndani
ya Ukumbi wa Bunge, Msigwa alipata nafasi ya kuuliza swali namba 115 lililokuwa
liulizwe na Joyce Mukya kuhusu Kampuni ya Kamwene Woodworks .
Godbless Lema |
Wabunge
wengine haikujulikana sababu za kutofika jana licha ya kuwa adhabu yao
ilikwisha tangu April 25 huku taarifa zikieleza kuwa Mbunge wa Arusha Mjini
Godbless Lema alikuwa kapelekwa mahakamani kujibu staka la uchochezi.
No comments:
Post a Comment