Mtoto mchanga alianguka kwa Bahati Mbaya ndani ya bomba la maji taka nchini China. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, May 30, 2013

Mtoto mchanga alianguka kwa Bahati Mbaya ndani ya bomba la maji taka nchini China.




Mtoto huyu alipewa

jina la 59 anaendelea

kupokea matibabu.
Mtoto mchanga aliyeokolewa kutoka ndani ya bomba la maji taka nchini China, alianguka ndani ya bomba hilo kwa bahati mbaya,kwa Mujibu wa Mama yake mtoto huyo amesema.





Mama huyo ambaye bado hajatajwa jila lake, aliwambia Polisi kuwa alijifungua Mwanawe akiwa chooni na kuwa mtoto huyo aliteleza na kuanguka ndani ya bomba hilo kwa bahati mbaya.




Mama huyo anaripotiwa kuangua kilio cha Kumpoteza mwanawe , licha ya kuwa  Mwanzoni hakukubali kuwa ni mwanawe hadi  baadaye.




Mtoto huyo anapatiwa  matibabu hospitalini baada ya kuokolewa kutoka ndani ya bomba la maji taka.




Bomba hilo lilikatwa kwa ustadi baada ya majirani kusikilia kilio cha mtoto huyo mjini Jinhua Jumamosi(May 26,2013).




Shirika la habari la Zhezhong, lilisema kuwa mama yake mtoto huyo mwenye umri wa miaka 22, aliwambia Polisi kuwa hangeweza kumudu gharama ya kulea mimba kwa Sababu Hajaolewa na aliiweka mimba yake kuwa siri kubwa.

 

Bomba aliloanguka ndani mtoto huyo.


Mtoto huyu alipewa jina la 59 anaendelea kupokea matibabu.




Alisema kuwa alijaribu kumzuia mtoto wake kuanguka baada ya kujifungua kwa ajali akiwa hospitalini lakini alianguka ndani ya bomba. 




Hata hivyo alimweleza mpangaji wake kulingana na shirika la habari la Xinhua.




Mama huyo alisema hakuwa na uwezo wa kumlea mwanawe kwa hivyo hakumwambia yeyote kuwa ni mwanawe.




Hata hivyo baadaye alijitambulisha na kuwambia Polisi ni mwanawe baada ya kuokolewa kwake.




Polisi wanachunguza ikiwa tukio hilo lilikuwa la ajali au kilikuliwa kitendo cha makusudi.




Mtoto huyo alipatikana ndani ya bomba lenye urefu wa nchi nne na alipata majeraha madogo kichwani na mikononi lakini anaendea kupata matibabu.




Kisa hicho kimezua mjadala mkali kwenye mitandao ya China huku baadhi wakisema kuwa mtoto huyo alikuwa ametupwa na mama yake kwa makusudi.



Sheria za China za kupanga uzazi ni kali mno huku familia ikiruhisiwa kuzaa mtoto mmoja pekee na wazazi wanaweza kuadhibiwa kwa kutozwa faini ikiwa watapatikana na hatia ya kupata zaidi ya mtoto mmoja.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad