Kanali Masawe atoa Miezi Sita kwa Viongozi wa Kiserikali na Vyama vya Siasa mkoani humo,kuwahamasisha wananchi Kujenga nyumba bora za Kuishi. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, May 15, 2013

Kanali Masawe atoa Miezi Sita kwa Viongozi wa Kiserikali na Vyama vya Siasa mkoani humo,kuwahamasisha wananchi Kujenga nyumba bora za Kuishi.


Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabiani Masawe amewataka Viongozi wa Wilaya Mkoani Humo ,ndani ya miezi sita kuhakikisha wanawahamasisha wananchi kwa kutumia rasilimali zilizopo hasa ardhi na misitu kujenga nyumba bora za kuishi kuliko zile za matembe kuonekana kuwa maskini bila kufanya kazi na kujiletea maendeleo.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabiani Masawe akiangalia moja ya nyumba siyobora wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo wilayani Biharamulo ,mkoani Kagera(Picha na Shabani Ndyamukama).


Mfano wa Nyumba bora ambazo Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabiani Masawe amewataka Viongozi wa Kiserikali na Vyama vya Siasa mkoani humo,kuwahamasisha wananchi Kujenga nyumba za mfano huo.



Mfano wa Nyumba bora ambazo Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabiani Masawe amewataka Viongozi wa Kiserikali na Vyama vya Siasa mkoani humo,kuwahamasisha wananchi Kujenga nyumba za mfano huo.


Mkuu wa Mkoa wa Kagera Kanali mstaafu Fabiani Masawe amewataka Viongozi wa Wilaya Mkoani Humo ,ndani ya miezi sita kuhakikisha wanawahamasisha wananchi kwa kutumia rasilimali zilizopo hasa ardhi na misitu kujenga nyumba bora za kuishi kuliko zile za matembe kuonekana kuwa maskini bila kufanya kazi na kujiletea maendeleo.




Makazi hayo yajengwe kwa kutumia matofali yasiyochomwa na kuezekwa kwa miti na nyasi kisha waongeze uzalishaji wa mazao ya kilimo na ufugaji ndani ya mwaka mmoja waezeke kwa mabati” Alisema Masawe.




Akiwa katika ziara ya kukagua Miradi mbalimbali ya Maendeleo katika wilaya za Biharamulo na Ngara mkoani humo, Kanali Masawe  alishauri ukusanyaji wa michango ya wananchi katika kujiletea maendeleo mkoani Kagera , uzingatie kutolewa rasilimali zinazopatikana katika mazingira yao kuliko madai ya fedha ambazo huliwa na watendaji wasio waaminifu katika Vijiji na Kata kwa kukosa kuwapatia stakabadi halali wala taarifa ya mapato na matumizi.




Aliwataka Maafisa ugani kuhakikisha wanafanya kazi zao Vijijini kuwasaidia utaalamu Wakulima na Wafugaji ikiwa ni  pamoja na Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri  kuwachukulia hatua Walevi saa za kazi pamoja na Wasiowajibika ipasavyo.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad