Beki wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Manchester United, Rio Ferdinand atangaza rasmi kustaafu soka la Kimataifa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, May 15, 2013

Beki wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Manchester United, Rio Ferdinand atangaza rasmi kustaafu soka la Kimataifa.



Rio Ferdinand.
Beki wa kimataifa wa Uingereza na klabu ya Manchester United, Rio Ferdinand ametangaza rasmi kustaafu soka la kimataifa kwa madai kwamba anataka kujihusisha zaidi na klabu yake.




Ferdinand mwenye umri wa miaka 34, ambaye ameichezea timu ya taifa ya Uingereza mechi 81 amesema kabla ya kutoa uamuzi huo alikiria kwa kipindi kirefu na kuona wakati wa yeye kustaafu soka la kimataifa umefika.




Ferdinand hajacheza mechi yoyote ya Uingereza toka katika mchezo wa kufuzu michuano ya Ulaya 2012 dhidi ya Switzerland Juni 2011 ambapo Roy Hodgson alimuita katika mechi ya kufuzu dhidi ya Kombe la Dunia dhidi ya San Marino na Montenegro Machi mwaka huu lakini alijitoa kwasababu ya kusumbuliwa na maumivu ya mgongo.




Nyota huyo ambaye ameisaidia klabu yake kunyakuwa taji la Ligi Kuu msimu huu amesema wakati wa kupisha damu changa katika timu ya taifa umefika ili naye aweze kupata nafasi ya kuongeza nguvu zake kuitumikia klabu yake.



RIO FERDINAND AKIWA NA TIMU YAKE YA UINGEREZA.



-1997: Aanza kuichezea England Mechi na Cameroon Uwanjani Wembley 

-1998: Ateuliwa Kikosi cha England Kombe la Dunia lakini hakucheza 

-2000: Atemwa Kikosi cha Euro 2000 

-2002: Aifungia England Bao walipoifunga Denmark 3-0 katika Kombe la Dunia

-2004: Afungiwa Miezi 8 kwa kukosa kupimwa Madawa yanayokatazwa 

-2006: Acheza Mechi 5 katika Kombe la Dunia huko Germany 

-2008: Awa Nahodha wa England kwa mara ya kwanza 

-2010: Terry avuliwa Unahodha na kukabidhiwa Ferdinand lakini ashindwa kucheza Fainali za Kombe la Dunia baada ya kuumia

-2011: Acheza Mechi yake ya 81 dhidi ya Uswisi kwenye Mchujo wa EURO 2012 

-2012: Atemwa EURO 2012 

-Machi 2013: Anaitwa tena kuichezea England Mechi za Kombe la Dunia lakini anajitoa kutokana na kukabiliana na majeruhi yake ya muda mrefu
-Mei 2013: Atangaza kustaafu kuichezea England 



Akiongelea kustaafu kwa Rio, Meneja wa England Roy Hodgson alisema: "Kwa kuwa Nahodha wa Nchi yake, kucheza Fainali za Kombe la Dunia 3, kunamfanya awemo katika kundi la Wachezaji spesho!."




Mara ya mwisho kwa Rio Ferdinand kuichezea England ilikuwa Juni 2011 walipocheza na Uswisi kwenye Mechi ya Mchujo ya EURO 2012.




Msimu huu, Ferdinand aliibuka upya baada ya kupona maumivu ya mara kwa mara aliyokuwa akipata huko nyuma, na kuiongoza Klabu yake Manchester United kutwaa tena Taji lao la Ubingwa wa Uingereza.




Akiongea, Rio Ferdinand alisema: “Nadhani huu ni wakati muafaka kung’atuka na kuwaachia Vijana na mimi nibakie kuichezea Klabu yangu tu.”




Kesho Alhamisi(May 16,2013), Roy Hodgson anatarajiwa kutangaza Kikosi cha England kitakachocheza Mechi za Kirafiki za Kimataifa na Republic of Ireland Uwanjani Wembley hapo Mei 29 na hapo Juni 2 kucheza huko Nchini Brazil Mjini Rio De Janeiro kwa kukabiliana na Brazil.




No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad