Leo
(April 13,2013) ndani ya Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Yanga waliichapa JKT
Oljoro kwa Bao 3-0 na kuzidi kujizatiti kileleni mwa Ligi Kuu Vodacom Tanzania
bara, wakiwa Pointi 6 mbele ya Timu ya Pili Azam FC yenye Pointi 46.
Ushindi
wa leo pia umeivua rasmi Simba SC Ubingwa kwa vile wana Pointi 35 na wamebakiza
Mechi 5 na hata wakishinda zote watafikisha Pointi 50 ambazo Yanga SC wameshazipita.
Mabao
yote ya Yanga SC yalifungwa Kipindi cha Kwanza -Dakika ya 5 na Nadir Haroub ‘Cannavaro’,-Dakika ya 19 Simon Msuva na -Dakika ya 43 Hamis Kiiza.
MSIMAMO:
NA
|
TIMU
|
p
|
W
|
D
|
L
|
GD
|
PTS
|
1
|
Yanga SC
|
22
|
16
|
4
|
2
|
28
|
52
|
2
|
Azam
FC
|
22
|
14
|
4
|
4
|
22
|
46
|
3
|
Kagera
Sugar
|
22
|
10
|
7
|
5
|
7
|
37
|
4
|
Simba
SC
|
21
|
9
|
8
|
4
|
11
|
35
|
5
|
Mtibwa
Sugar
|
23
|
8
|
9
|
6
|
2
|
33
|
6
|
Coastal
Union
|
22
|
8
|
8
|
6
|
3
|
32
|
Ligi hiyo ya VPL itaendelea kesho (April 14,2013) Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam kwa Mechi ngumu kati ya Simba SC na Azam FC na kipigo kwa Azam FC kitaifagilia Yanga SC kutwaa Ubingwa.
Katika
hatua Nyingine Mechi tano kati ya sita za Super Week za Ligi Kuu ya
Vodacom zilizokuwa zioneshwe moja kwa moja (live) na Kituo cha televisheni cha
SuperSport cha Afrika Kusini sasa hazitaoneshwa kutokana na matatizo ya
kiufundi.
Kwa
mujibu wa Mtayarishaji Mtendaji (Executive Producer) wa SuperSport Kanda ya
Afrika, Max Tshunungwa ambaye yuko nchini, wameshindwa kuonesha mechi hizo
kutokana na matatizo ya kiufundi katika magari yao ya kurushia matangazo (OB
van) yanayohudumia Afrika Mashariki- Kenya, Tanzania na Uganda.
Mechi
hizo ni kati ya Azam na African Lyon, Yanga na Oljoro JKT, Azam na Simba,
Coastal Union na JKT Ruvu na Mgambo Shooting na Yanga itakayochezwa Aprili 17
mwaka huu jijini Tanga.
Tatizo
hilo pia limeathiri mechi za Ligi Kuu ya Kenya (KPL) ambazo hazitaonekana
wikiendi hii. SuperSport ndiyo yenye haki za matangazo ya televisheni kwa ligi
hiyo ya Kenya.
Tshunungwa
amekutana na Sekretarieti ya TFF na Kamati ya Ligi kuelezea tatizo hilo.
SuperSport kwa kushirikiana na Kamati ya Ligi na TFF watapanga mechi nyingine
za Super Week kabla ya ligi kumalizika msimu huu.
Pia
TFF, Kamati ya Ligi na SuperSport watakuwa na mkutano mfupi wa waandishi wa
habari wakati wa mapumziko kwenye mechi ya leo kati ya Yanga na Oljoro JKT
kwenye Uwanja wa Taifa.







No comments:
Post a Comment