PICHA: Rulenge Voleball ikifungwa Vikapu 48 kwa 36 na Ngara Voleball huku Ngara Starz nao wakipokea kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Mukombozi FC ya Muleba,katika uwanja wa Kokoto Mjini Ngara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, April 15, 2013

PICHA: Rulenge Voleball ikifungwa Vikapu 48 kwa 36 na Ngara Voleball huku Ngara Starz nao wakipokea kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Mukombozi FC ya Muleba,katika uwanja wa Kokoto Mjini Ngara.


Timu ya mpira wa kikapu Rulenge  jana imeonja joto ya jiwe baada ya kufungwa Vikapu 48 kwa 36 kutoka kwa timu ya mpira wa kikapu ya Ngara.


Mchezo huo ukichezwa katika uwanja wa mpira wa kikapu mjini Ngara ,timu zote zilionekana kushambuliana kwa zamu lakini Ngara walionekana kuutumia vema uwanja wao wa nyumbani kuwapa raha ya magoli mashabiki wao.


Kutokana na ushindi huo wa vikapu 48 kwa 36 …Akisoni Masanja amsema walitaraji ushindi huo kutokana na kujituma pamoja na mazoezi waliyokuwa wakiyafanya  kujianda na mchezo huo.


Nae Padri Joni Bosco akiwaongoza vijana wake  wa Rulenge katika mchezo huo amesmea kilicho waangusha na kufungwa vikapu hivyo ni tatizo la ugeni wa uwanja na pia kuiomba Serikali wilayani Ngara kuweka mikakati ya Kuendeleza mchezo huo wa Kikapu .


Ngara Basket Ball Squard.

Rulenge  Basket Ball Squard.

Rulenge  Basket Ball Squard.

Timu zote zikiwa Uwanjani tayari kwa mchezo ambapo Ngara Basket Ball walishinda kwa Vikapu 48 -36.


Kikosi cha Ngara starz kikiwa katika picha ya pamoja katika uwanja wa Kokoto mjini Ngara,tayari kwa mchezo dhidi ya Mukombozi FC kutoka wilayani Muleba ambapo wageni Mukombozi FC walishinda bao 1-0.
Refari wa mchezo kati ya   Ngara starz   dhidi ya Mukombozi FC kutoka wilayani Muleba ,Seif Omary Upupu ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa chama cha soka wilayani ngara NDFA, wageni Mukombozi FC walishinda bao 1-0.
Kikosi cha Mukombozi FC  kikiwa katika picha ya pamoja katika uwanja wa Kokoto mjini Ngara,tayari kwa mchezo dhidi ya Mukombozi FC kutoka wilayani Muleba ambapo wageni Mukombozi FC walishinda bao 1-0.

Timu ya Ngara starz hapo jana (April 14,2013)  imekubali  kufumuliwa bao 1 -0  katika uwanja wake wa Nyumbani  wa Kokoto,uliopo mjini Ngara ,kutoka kwa wageni  timu ya Mukombozi FC ya  wilayani  Muleba  ambayo ilikuja kucheza mchezo huo wa kirafiki pamoja na kudumisha Ujirani mwema baina ya timu hizo mbili.


Katika mchezo huo  goli hilo moja la wageni Mukombozi FC lilifungwa na mchezaji wao Renatus Jeremia  na kumfanya kocha wa timu hiyo Dioniz  Mutechura  kusema kuwa Ngara starz wangewafunga magoli mengi ila uchovu wa safari kutoka Muleba hadi Ngara ndio uliowafanya kucheza chini ya kiwango.


Kwa upande wake Kiongozi wa Ngara Starz –Baraka Abbas amesema wamekubali  kipigo hicho na kusema kuwa  bado wako  katika mikakati ya kuijenga timu yao .


Aidha Mwenyekiti wa Klabu ya Mukombozi FC  Nalisisi Paulo  ameishukuru timu ya Ngara starz kwa mapokezi mazuri waliyowapatia na kuwapa   mwaliko wa kuwatembelea  lengo ni  kudumisha urafiki wao wa kimichezo kwa Ngara starz  na Mukombozi FC.
Mashabiki wakifatilia  mchezo huo  katika uwanja wa Kokoto mjini Ngara,ambapo timu ya  Mukombozi FC kutoka wilayani Muleba walishinda  bao 1-0 dhidi ya Ngara Starz.
Kikosi cha  timu ya Ngara Voleball  kikiwa katika  katika mazoezi ya kupasha kujiandaa na mchezo wake dhidi ya Rulenge Voleball ambapo Rulenge walishinda mchezo huo kwa Seti 3 - 0 .
Rulenge Voleball  wakijianda kuingia uwanjani  kupambana na wenyeji wao Ngara Voleball ambapo Rulenge walishinda mchezo huo kwa Seti 3 - 0 .
Mashabiki wakifatilia mchezo kati ya Ngara Voleball dhidi ya Rulenge Voleball ambapo Rulenge walishinda mchezo huo kwa Seti 3 - 0 .
Mashabiki wakifatilia mchezo kati ya Ngara Voleball dhidi ya Rulenge Voleball ambapo Rulenge walishinda mchezo huo kwa Seti 3 - 0 .


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad