Anna Kibira Mwenyekiti Mpya Chama cha Netiboli nchini (CHANETA) . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, April 21, 2013

Anna Kibira Mwenyekiti Mpya Chama cha Netiboli nchini (CHANETA) .


Anna Kibira
Anna Kibira amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Netiboli nchini (CHANETA) Katika uchaguzi uliofanyika jana (April 20,2013) Mkoani Dodoma.



Kibira alikuwa Katibu Mkuu katika uongozi uliomaliza muda wake, lakini mwanzoni tu mwa uongozi huo alisimamishwa kwa muda usiojulikana kwa madai ya utovu wa nidhamu.




Katika uchaguzi wa jana, Kibira alimuagusha Mbunge wa Afrika Mashariki Shyrose Bhanji. Bhanji alikuwa Makamu Mwenyekiti katika uongozi uliomaliza muda wake.




Kibira aliibuka na ushindi kwa kura 61 dhidi ya 21 za mpinzani wake huku Zainab Mbiro ambaye mara kadhaa amekuwa akigombea lakini hachaguliwi, safari hii alibahatika kuchaguliwa kuwa  Makamu Mwenyekiti wa CHANETA.




Akitangaza matokeo hayo, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi Betty Mkwassa alisema, mpinzani wa Mbiro Agnes Mangasila alipata kura 25 dhidi ya 57 za Mbiro.




Agness Hatibu aliyekuwa peke yake kwenye nafasi ya Mweka Hazina, alipata kura 66 huku kura 17 zilimkataa.




Wajumbe walionekana kutaka sura mpya kwani waliwatosa wale waliokuwa kwenye uongozi uliomaliza muda wake ambao ni Mary Protas, Mwajuma Kisengo na Rose Kisiwa na kuwachagua Yasinta Silvester, Fortunata Kabeja, Asha Sapi, Penina Igwe, Hilder Mwakatobe na Judith Ilunda katika nafasi za ujumbe wa Kamati ya Utendaji.




Mapema kabla ya uchaguzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dk Rehema Nchimbi alitoa changamoto kwa uongozi mpya CHANETA kuhakikisha wanaweka kanuni na viwango ili kuondokana na migogoro isiyo ya lazima kwa ajili ya manufaa ya mchezo huo.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad