Akutwa kando ya barabara akiwa amepoteza maisha huku akiwa na mfuko wa mahindi kilo 20 katika kijiji cha Rwinyana wilayani Ngara mkoani Kagera. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, April 07, 2013

Akutwa kando ya barabara akiwa amepoteza maisha huku akiwa na mfuko wa mahindi kilo 20 katika kijiji cha Rwinyana wilayani Ngara mkoani Kagera.



wilayani Ngara
Mtu mmoja anayekadiliwa kuwa na umri wa miaka 53 amekutwa amekufa katika barabara  ielekeayo  mgodi wa  madini ya Nickel -Kabanga katika kijiji cha Rwinyana wilayani Ngara mkoani Kagera.




Afisa mtendaji wa kijiji cha Rwinyana Bw.Venace Jonh  amemtaja mtu huyo kuwa Jeremo Onesimo mkazi wa kitongoji cha Nageli kijijini humo.




Amesema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia leo baada ya mtu huyo kukutwa kando ya barabara akiwa amepoteza maisha huku akiwa na mfuko wa mahindi kilo 20.




Kijana wa marehemu huyo Nuwaka Pambano amesema awali baba yake huyo alikwenda kusaga jana jioni kilomita 2 kutoka nyumbani baada ya hapo alianguka kutokana  na  pombe alizokuwa amekunywa.




Kufuatia hali hiyo kijana huyo alimsogeza kando ya barabara ili arudi nyumbani na ndipo alimwambia akipata nguvu atarudi nyumbani ambapo baadae amekutwa  amefariki dunia.




Jeshi la polisi wiyalani  Ngara  limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.  

   

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad