Mabingwa wa Tanzania Bara, Simba SC wang'olewa kwa 4 – 0 + 1 – 0 katika michuano ya Klabu Bingwa Africa huku Azam FC ikiua 5 – 0 + 3 – 1 na kuwa timu pekee iliyobaki kwenye michuano ya Afrika. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, March 03, 2013

Mabingwa wa Tanzania Bara, Simba SC wang'olewa kwa 4 – 0 + 1 – 0 katika michuano ya Klabu Bingwa Africa huku Azam FC ikiua 5 – 0 + 3 – 1 na kuwa timu pekee iliyobaki kwenye michuano ya Afrika.



Azam FC
Kama ilivyotarajiwa na wengi, Azam FC ndio timu pekee iliyobaki kwenye michuano ya Afrika  baada ya jioni ya leo(March 03,2013) kuifunga Al Nasir ya Juba, mabao 5 - 0 kwenye Uwanja wa Juba, Sudan Kusini.





Kwa matokeo hayo, Azam FC  inaingia Raundi ya Pili ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa ushindi wa jumla wa mabao 8 - 1, kufuatia ushindi 3 - 1 katika mchezo wa kwanza wiki mbili zilizopita Dar es Salaam.



Azam FC sasa itamenyana na mshindi kati ya Al Nasir ya Libya na El Khartoum El Watan ya Sudan. 



Aidha Kuna uwezekano mkubwa Azam FC ikarejea Sudan, kwani katika mchezo wa kwanza, Al Nasir ililazimishwa sare ya bila kufungana na El Khartoum El Watan.




Katika mchezo huo, mabao ya Azam FC  yalifungwa na Kipre Herman Tchetche, John Raphael Bocco kila mmoja mawili, moja kila kipindi na lingine Khamis Mcha ‘Vialli’.




Mapema jioni ya leo(March 03,2013, Jamhuri ya Pemba, imekuwa timu ya kwanza ya Tanzania kuaga michuano ya Afrika, baada ya kufungwa mabao 5-0 na wenyeji  Kedus Giorgis nchini Ethiopia katika mchezo wa marudiano, Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika.




Matokeo hayao, yanamaanisha, Jamhuri imeaga kwa kufungwa jumla ya mabao 8-0, baada ya awali kutandikwa 3-0 katika mchezo wa kwanza Uwanja wa Gombani, Pemba.



Simba SC
Wawakilishi wengine wa Bara katika michuano hiyo na Mabingwa watetezi wa Ligi kuu soka Vodacom Tanzania Bara , Simba SC wametolewa baada ya kufungwa mabao 4-0  na  Recreativo de Libolo ya Angola kwenye Uwanja wa Manispaa mjini Calulo, Angola.




Matokeo hayo  yanaifanya Simba SC  itolewe kwa jumla ya mabao 5-0, baada ya awali kufungwa bao 1-0 Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad