CHADEMA na kugatua madaraka kwa kutafsiri sera yake ya majimbo, ukianza kazi rasmi katika kanda zake 10 huku Mbeya M4C ikivunja Rekodi . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, March 03, 2013

CHADEMA na kugatua madaraka kwa kutafsiri sera yake ya majimbo, ukianza kazi rasmi katika kanda zake 10 huku Mbeya M4C ikivunja Rekodi .


 Sehemu ya Babango kwenye mkutano huo.

Maandamano  ambayo yaliongozwa na Mbowe yaliyoanzia katika eneo la Uhasibu Mafiat hadi katika Uwanja wa Ruanda Nzovwe,Mbowe aitembea kwa mwendo wa kilomita tano ambapo makundi ya waendesha bodaboda, baiskeli na watembea kwa miguu walijitokeza kwa wingi kuunga mkono maandamano hayo.



Chama  cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kuwa kimeamua kuanza kutekeleza sera yake ya kuongoza kwa majimbo sasa ili kuongeza nguvu ya mapambano na harakati za kuhakikisha wanafanikisha malengo yao ya kushika dola mwaka 2015, badala ya kuendelea kutumia mfumo wa zamani ambao ilikuwa rahisi kudhibitiwa na serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) .


 

Kadhalika, chama hicho kimesema hakitampokea mwanachama yeyote wa Chama Cha Mapinduzi atakayekosa nafasi ya kugombea kwenye chama chake na kutimkia Chadema katika dakika za mwisho kuelekea kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2015.




Chama cha Demokrasia

na Maendeleo CHADEMA

kimesema kuwa kitalazimisha

 maandamano nchi nzima

iwapo Waziri wa Elimu na

 Mafunzo ya Ufundi na Naibu

 wake hawatakubali kujiuzulu

kwa kusababisha anguko la

 elimu nchini.
Mwenyekiti wa Chadema taifa, Freeman Mbowe aliyasema hayo wakati akizungumza na viongozi wa Chadema wa mikoa ya Nyanda za Juu Kusini ikiwa ni maandalizi ya kuzindua kanda yake kwenye kanda hiyo.




Alisema kuwa mfumo wa zamani ambao mambo yote ya harakati za chama hicho yalianzia makao makuu ya chama,  ulikuwa ni rahisi kudhibitiwa na dola ya CCM kwa kuwa walikuwa wakiwavizia viongozi wa kitaifa wanapotoka nje kwenda kuendesha harakati wanawapiga mabomu, kuwakamata na kuwafungulia kesi mahakamani.




Tunataka dola ikusubiri viongozi wa kitaifa watoke makao makuu ili wawadhibiti, wasikie mapambano yanatokea kwenye kanda zetu kama hii ya Nyanda za Juu Kusini, kanda ya Magharibi na nyinginezo,” alisema Mbowe.




Alisema kuwa katika mabadiliko hayo pia Chadema inaachana na siasa za kiuanaharakati na badala yake inaanza kujikita kwenye siasa za maandalizi ya kushika dola.




Akizungumzia utaratibu wa baadhi ya wanachama wa vyama vingine, kikiwemo chama tawala CCM kukimbilia ndani ya chama hicho baada ya kutoswa kwenye nafasi za uchaguzi, Mbowe amesema kuwa kuanzia sasa Chadema hakitampokea mwanachama yeyote wa aina hiyo.





Sehemu ya maelfu ya

 wananchama wa chadema

mkoani mbeya wakimsikiliza

mwenyekiti wa chadema na

mbunge wa  Hai
Freeman Mbowe
Mbowe alisema kuwa Chadema hivi sasa ipo kwenye maandalizi makubwa ya kunyakua dola mwaka 2015 na hivyo inao wajibu wa kuwaandaa wanachama wake ipasavyo ili kiweze kuwa na wagombea wazuri, imara na wenye uwezo wa kuwezesha chama hicho kupata ushindi mkubwa.




Kama kuna mtu leo anakula matunda ya ufisadi ndani ya Chama Cha Mapinduzi akidhani kuwa atahamia Chadema kwa kuwa ana fedha za kununua kura za maoni, ameula wa chuya, hatutampokea mtu wa aina hiyo, ” alisema Mbowe.




Alisema kuwa kuanzia sasa Chadema itawapokea wanachama kutoka vyama vingine baada ya kuwapima uadilifu wao, kuchunguza historia yao na utayari wao wa kutumika ndani ya chama ili waweze kupata wanachama na viongozi wazuri watakaokisaidia chama kushika dola mwaka 2015.




Alisema kuwa Chama Cha Mapinduzi kimekuwa kikitumia mbinu mbalimbali za kukisambaratisha Chadema, ikiwa ni pamoja na kuwatumia mamluki ndani ya chama, lakini kutokana na uimara wa Chadema mbinu hizo zimekwama na Chadema inasonga mbele.





Sehemu ya maelfu ya

 wananchama wa chadema

mkoani mbeya.
Mbowe ambaye pia ni kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni alisema kuwa yeye pamoja na wapambanaji wenzake wametumia zaidi ya miaka 20 kuijenga Chadema na kuipa nguvu kisiasa hadi hapo na hivyo hatakubali kuruhusu chama hicho kihujumiwe au kusambaratishwa kwa namna yoyote ile.




Alisema kuwa ikiwa wana-Chadema wataruhusu Chadema ife leo, itawachukua tena miaka 20 mingine kuijenga na kuifikisha mahali iilipo hivi leo.




Mbowe alitolea mfano wa vyama vya siasa vilivyowahi kupata nguvu na umaarufu mkubwa wa kisiasa nchini kama vile Chama cha Wananchi, CUF, NCCR – Mageuzi na TLP ambavyo alidai kuwa CCM illifanikiwa kuvizima na kuwa hata vyenyewe itavichukua muda mrefu usiopungua miaka 20 kurejesha umaarufuvilivyokuwa nao.




Mbunge wa iringa mjini Chadema Mchungaji Peter Msigwa akiunguruma kwneye mkutano wa chadema Mbeya.

 Mbunge wa Mbeya mjini Chadema Joseph Mbilinyi aka Mr II Sugu akiwasha moto kwenye mkutano wa Chadema Mkoani Mbeya.

 Sehemu ya Michango mbalimbali kutoka kwa wanachama na wapenzi wa chadema waliochangia kampeni ya vuguvugu la mabadiliko (M4C)kwenye mkutano huo wa hadhara.




Katika Hatua Nyingine  Kanda ya Ziwa Magharibi imetangaza kikosi kazi kilichosheni wataalamu wa fani mbalimbali ili kuanza Utekelezaji kwa Vitendo mkakati wa  Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kugatua madaraka kwa kutafsiri sera yake ya majimbo, umeanza kazi rasmi katika kanda zake 10. 




Freeman Mbowe.
Kanda hiyo inayohusisha mikoa ya Geita, Kagera na Mwanza, ilizinduliwa wiki iliyopita mkoani Mwanza, mbele ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe.




Mkutano wa uzinduzi wa kanda hiyo uliohudhuriwa na wajumbe wa mabaraza ya uongozi, wabunge na madiwani kutoka mikoa hiyo, uliwachagua watu sita kuunda timu ya muda ya uratibu wa kanda kwa miezi mitatu.




Waliochaguliwa kuongoza kanda hiyo ni Peter Mekere (Mwenyekiti), Dk. Rodrick Kabangila (Makamu Mwenyekiti), Renatus Bujiku (Katibu), Cecilia Odemba (Mhazini) na Tungaraza Njugu.




Mekere ni mtaalamu mshauri wa biashara na utawala na mafunzo ya biashara. Ana shahada ya biashara na uongozi na stashahada ya ualimu. Ni mwenyekiti wa kamati ya fedha na mipango ya Shirika la nyumba la Taifa (NHC), Kanda ya Ziwa.




Kabangila ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Afya, Bugando, daktari bingwa wa magonjwa ya binadamu na Makamu wa Rais wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT).




Ana shahada ya uzamili ya magonjwa ya wanadamu, shahada ya udaktari, shahada ya uzamili, epidemilojia na utafiti wa huduma za afya.




Bujiku ni mwalimu, mtaalamu mshauri, ofisa wa kanda ya ziwa wa shirika la ACORD kwa muda sasa.




 Ana shahada ya uzamili, uongozi na mipango, shahada ya Elimu, Stashahada ya Maendeleo na misaada ya kiutu.




Njugu amekuwa Meneja wa shirika la kijamii (CACT-Mwanza 2008-2010), meneja wa Chama cha Akiba na Mikopo (MWAUWASA SACCOS 2007 hadi sasa) ana cheti cha uhasibu kutoka Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino (SAUT) na cheti cha sheria kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.




Odemba ni Meneja masoko katika usafiri wa anga, mkurugenzi wa kampuni ya uwakala ya usafiri wa anga, na amewahi kuwa katibu wa kamati ya uhamasishaji ya vuguvugu la mabadiliko (M4C) kanda ya Ziwa.




Mekere alisema: “Timu yetu imetokana na watu wenye taaluma mbalimbali ambao wamekuwa wakitafuta nafasi kukisaidia chama kupitia taaluma zao.




Tunaipongeza CHADEMA kwa kuanzisha sera ya majimbo kuandaa Watanzania kupata maendeleo kwa haraka kwani utaratibu huu wa majimbo ya chama unarudisha mamlaka kwa wananchi, na ni maandalizi ya kuongoza nchi.




Kwa utaratibu huu wananchi wamerudishiwa madaraka yao, wana nafasi ya kuamua kuhusu rasilimali zao na kupanga namna ya kuzitumia. Utaratibu huu unaharakisha maendeleo tofauti na mfumo wa kimikoa uliowekwa na CCM.”

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad