Yanga SC ni ushindi tuu - yafikisha pointi 42 na kumuacha Bingwa Mtetezi Simba SC kwa Pointi 11 . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, February 27, 2013

Yanga SC ni ushindi tuu - yafikisha pointi 42 na kumuacha Bingwa Mtetezi Simba SC kwa Pointi 11 .




Yanga SC
v/s
Kagera Sugar.
Kwa mara ya pili mfululizo, kiungo Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima leo(Feb 27,2013) tena amekuwa shujaa wa timu yake ya  Yanga SC baada ya kuifungia bao pekee la ushindi katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.




Niyonzima alijikuta akituzwa fedha na mashabiki wa timu yake baada ya mechi hiyo, iliyokuwa ngumu kwa Wana Jangwani, kutokana na kuibeba timu hiyo mara mbili mfululizo kwa kufunga mabao ya juhudi binafsi, ikiwemo mechi iliyopita dhidi ya Azam FC. 




Ushindi huo unaifanya Yanga SC ifikishe pointi 42, baada ya kucheza mechi 18, hivyo kujitanua kileleni mwa Ligi Kuu, ikiizidi Azam FC kwa pointi sita, ambayo inashika nafasi ya pili kwa pointi zake 36, wakati mabingwa watetezi, Simba SC wanashika nafasi ya tatu wakiachwa Pointi 11 kwani wana Pointi zao 31.



Kagera Sugar  inabaki na pointi zake 28 katika nafasi ya tano, baada ya kucheza mechi 19, chini ya Coastal Union ya Tanga inayoshika nafasi ya nne kwa pointi zake 30.




Hata hivyo, mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Didier Kavumbangu aliikosesha timu yake bao, baada ya kupiga juu ya lango mkwaju wake wa penalti dakika ya 44.




Refa Mberwa, alitoa penalti hiyo baada ya Kavumbangu mwenyewe kudakwa miguu kwenye eneo la hatari na kipa wa Kagera, Mganda Hannington Kalyesebula.



Aidha Kwa ushindi huo, Yanga imelipa kisasi cha kufungwa 1-0 na Kagera katika mchezo wa kwanza wa ligi hiyo, mwishoni mwa mwaka jana mjini Bukoba.




Matokeo Mengine ya Ligi Kuu soka Vodacom Tanzania Bara:-





Castal Union  0 – 0 Ruvu Shooting.



Mtibwa Sugara 0 – 0 Tanzania Prisons.




REKODI YA WACHEZAJI WAPYA YANGA SC:


MCHEZAJI                      MABAO  MECHI


Said Bahanuzi Yanga      13           20          3penalti


D. Kavumbangu Yanga   10            22          1penalti


Simon Msuva Yanga        5             22


Nizar Khalfan Yanga        4             13


Mbuyu Twite Yanga         3             18
 

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad