Full HD barcelona vs real madrid 1-3 goals & highlights 27/02/2013 - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Wednesday, February 27, 2013

Full HD barcelona vs real madrid 1-3 goals & highlights 27/02/2013




Wakiwa Nyumbani  NOU CAMP, FC Barcelona walichapwa Bao 3-1 na Mahasimu wao wakubwa Real Madrid na kutupwa nje ya COPA del REY na leo Nyota wao Lionel Messi alishindwa kufanya Mazoezi na wenzake na Madaktari wa Klabu yake kulazimika kwenda Nyumbani kwake na kumgundua ni mgonjwa na ana Homa.



Taarifa iliyotoka kwenye Tovuti ya Barcelona imetamka kuwa Staa huyo alitibiwa na Madaktari wao na kumshauri apumzike.



Jana Messi alicheza Dakika zote 90 za kipigo chao toka kwa Madrid  na Barcelona na wanaamini atakuwa fiti kucheza Mechi ya La Liga hapo Jumamosi Uwanjani Santiago Bernabeu dhidi ya Real Madrid.





Barcelona imethibitisha Alhamisi ni Siku ya Mapumziko kwa Wachezaji na Ijumaa watarudi Mazoezini ambako Messi anategemewa kuhudhuria.



Msimu huu, Messi ameichezea Barcelona  katika kila Mechi ya La Liga na kuiwezesha kuwa kileleni wakiwa Pointi 16 mbele ya Real Madrid ambao ni Mabingwa watetezi.



Wakati huo huo, Beki wa Barcelona, Jordi Alba, ambae jana ndie alifunga Bao pekee la Barca walipochapwa 3-1 na Real Madrid - ameeleza kuwa ana imani kwamba kutolewa kwao nje ya COPA del REY kutawaimarisha katika Mechi ya Marudiano ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, ambapo watacheza Uwanjani Nou Camp na AC Milan ambao wanatinga hapo wakiwa Washindi katika Mechi ya kwanza kwa Bao 2-0.



Wiki iliyopita, katika Mechi ya kwanza iliyochezwa San Siro, Bao za Kipindi cha Pili za Kevin-Prince Boateng na Sulley Muntari, ziliwapa AC Milan ushindi wa Bao 2-0 dhidi ya Barca na Timu hizi zitarudiana Nchini Spain hapo Machi 12.



Alba ametamka: “Jana tulicheza kwa nguvu zote lakini haikuwa na kipigo hiki kitatupa nguvu kuivaa AC Milan. Tumefungwa Mechi mbili muhimu na ni muhimu tupate Goli la mapema.”

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad