Radio hizi
mbili (Radio
IMANI na Kwa NEEMA FM ) zimefungiwa miezi sita, na Clouds FM kupigwa faini ya milioni 5.
Radio Kwa NEEMA FM ya Jijini Mwanza:- Sababu ni kushabikia maswala ya uchinjaji Mwanza.
Radio Iman
FM ya Morogoro: Kushabikia watu kutoshiriki Sensa 2012.
Na Radio Clouds FM ya Jijini Dar es salaa,:-Kuendesha/kushabikia
masuala ya ushoga wakati wa uchaguzi wa Marekani, kuendesha kipindi cha
uchochezi wakati wa uchaguzi wa Marekani.
-Kuendesha
kipengere cha 'Jicho la ng'ombe' kisichofuata maadili.
Akizungumza na waandishi wa habari leo (feb 26,2013)jijini Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Walter Bgoya alisema Kituo cha Clouds FM kimetakiwa kufuta kipindi chake cha Jicho la Ng'ombe mara moja pamoja na kulipa faini ya sh. milioni 5.
Makamu
Mwenyekiti wa
Kamati
ya Maadili ya
Utangazaji
nchini,
Walter
Bgoya (katikati),
akizungumza
na wanahabari
leo
jijini Dar es Salaam
ukumbi
wa habari Maelezo.
|
Akizungumza na waandishi wa habari leo (feb 26,2013)jijini Dar es Salaam, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Walter Bgoya alisema Kituo cha Clouds FM kimetakiwa kufuta kipindi chake cha Jicho la Ng'ombe mara moja pamoja na kulipa faini ya sh. milioni 5.
Kituo cha
Clouds FM kimetakiwa kutoanzisha kipindi kingine kinacho fanana na Jicho la
Ng'ombe.
Akifafanua
zaidi Makamu Mwenyekiti huyo alisema vituo vya Imani FM na Kwa-Neema vimefungiwa
kwa kosa la kufanya kazi zao kwa uchochezi jambo ambalo ni kinyume cha maadili
ya tasnia ya utangazaji.
Gari
la Kituo cha
Imani
FM kilichofungiwa
likiwa Idara ya Habari Maelezo leo.
|
Kituo cha Imani FM kinadaiwa kufanya uchochezi kwa
wananchi juu ya suala la sensa ya watu na makazi huku kile cha Kwa-Neema
kufanya uchochezi juu ya mgogoro wa uchinjaji wanyama kwa Waislamu na Wakristu
mkoani Geita.
Hata hivyo
Kamati ya Maadili imeweka mlango wazi kwa vituo hivyo kukata rufaa endapo havikuridhika
na adhabu vilivyo pewa kutokana na makosa vinao daiwa kufanya.
Kamati
Imevitaka vyombo vyote vya habari kufanya kazi kwa kuzingatia Kanuni Sheria na
maadili ya tasnia hiyo ili kuepuka kuzua migogoro kwa wananchi ambao wamekuwa wakiviamini
vituo hivyo.
Hata hivyo
mara baada ya ujumbe wa kamati hiyo kumaliza kusoma adhabu hizo kwa waandishi
wa habari haukuruhusu maswali kwa waandishi wa habari, hivyo waandishi kubaki
wameduwaa.
SOURCE: Jamii
Forums
No comments:
Post a Comment