Baada ya matokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne 2012: Wakuu wa shule wadai ilitungwa kwa mfumo tofauti. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, February 25, 2013

Baada ya matokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne 2012: Wakuu wa shule wadai ilitungwa kwa mfumo tofauti.


Baada ya matokeo

mabaya ya

mtihani wa kidato

cha nne  2012.
Matokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne yamezidi kuibua mapya, baada ya wamiliki wa shule na vyuo binafsi nchini kusema mitihani ilitungwa kwa mfumo tofauti na uliozoeleka miaka yote, huku tume iliyounndwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda ikipondwa na baadhi ya watu.


 

Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Shule na Vyuo Binafsi nchini (TAMONGSCO), Mahmoud Mringo alisema kwamba maswali waliyoulizwa watahiniwa yalikuwa ya kujieleza tofauti na miaka ya nyuma, ambapo mfumo uliotumika uliwataka watahiniwa kutaja vitu tu bila ya kulazimika kuvielezea kwa undani.




Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi

Dk Shukuru Kawambwa
Kauli yake iliungwa mkono na Mkuu wa Taaluma katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Marian, Florence Mapunda ambaye alisema kuwa mtihani wa mwaka jana ulitaka zaidi watoto kujieleza tofauti na miaka ya nyuma wakati wanafunzi walipokuwa wanakariri.



Hata hivyo, Msemaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (Necta), John Nchimbi alisema mfumo wa mtihani haukubadilika kwa namna yoyote na kuwa upo kama ule wa miaka yote.



Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philip Mulugo, kwa upande wake alisema madai yanayotolewa hayana msingi, huku akihoji kwa nini yasitoke tangu mitihani ilipokuwa ikifanyika na badala yake yanatoka baada ya kutangazwa kwa matokeo.



Matokeo ya mtihani wa kidato cha nne uliofanyika mwaka jana yanaonyesha kuwa watahiniwa 240,903 sawa na asilimia 60.6 wamepata sifuri, huku wanafunzi 23,520 tu ambao ni sawa na asilimia 5.16 ndiyo waliofaulu na wengine 103,327 sawa na asilimia 26.02 wamepata daraja la nne.



Waziri Mkuu Pinda
Kutokana na matokeo hayo, Waziri Mkuu Pinda, juzi alitangaza kuunda tume ya kuchunguza chanzo cha matokeo hayo kuwa mabaya, hatua ambayo hata hivyo imekosolewa na wasomi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).



Tume hiyo inayoundwa na wajumbe kutoka Taasisi za Elimu, Chama cha Waalimu, Kamati ya Bunge ya Huduma za Jamii na Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (Tahossa) inatarajiwa kuanza kazi wiki hii.



Profesa Gaudence Mpangala wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam alisema kuunda tume ni kupoteza muda kwa sababu matatizo na changamoto zote ndani ya sekta hiyo yanajulikana, huku mwenzake, Profesa Chriss Maina pia wa UDSM akisema kuunda tume hakutaisaidia kwa kuwa Serikali inaidharau sekta ya elimu.



Mbatia
Tatizo ni kutowekeza kikamilifu katika sekta ya elimu, imekuwa na matumizi makubwa katika mambo yasiyokuwa ya lazima,”alisema Profesa Mpangala.



Alisema matatizo mengine ni mazingira magumu ya kufundisha na uhaba wa walimu. “Kinachotakiwa wajipange kufanyia kazi changamoto hizi zilizopo badala ya kuunda tume, wakati fedha nyingi tunasikia inapotea kwenye ubadhirifu,”alisema Profesa Mpangala.



Naye Profesa Maina alisema: “Hiyo tume ya kazi gani kwa sababu matatizo yanafahamika wazi, umewahi kusikia taifa gani ambalo halina mtalaa wa elimu. Hiyo ndiyo hali halisi kwa nchi yetu. ”





Dk. Slaa
Dk. Slaa alishangazwa na hatua hiyo ya Waziri Mkuu kuunda tume kwa ajili ya kufuatilia kufeli kwa wanafunzi, akisema ni juzi tu Bunge limemaliza kikao chake Dodoma na kuitupilia mbali hoja binafsi ya Mbatia.





Alisema hoja binafsi ya Mbatia ilikuwa na nia ya kupitisha azimio la Bunge kuunda kamati teule ya kuchunguza tatizo la udhaifu katika sekta ya elimu, lakini kwa ushabiki wa wabunge wa CCM akiwemo Waziri Mkuu, ilikataliwa.



Naye Dk. Bana alimbeza Pinda kwa hatua hiyo ya kuunda tume kwa masuala ya mtihani, akisema tatizo la kufeli kwa wanafunzi halihitaji tume kwani kasoro ziko wazi.



Alisema kuwa matatizo ya walimu yanajulikana, huku serikali ikijidanganya kutengeneza sera ya elimu kinyemela bila kushirikisha wataalamu.





ALAMA ZA JUMLA ZA UFAULU WA MTIHANI WA TAIFA KIDATO CHA NNE 2012.



Div 1 =1,641.

Div 2 =6,453.

Div 3 =15,426.

Div 4 =103,327.

Div 0 =243,903.
 
 



Habari Na:Mwananchi.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad