![]() |
Sensa ya Watu na Makazi. |
Aidha
matokeo hayo ya Sensa ya Watu na Makazi iliyofanyika nchini Agosti 26 hadi
Septemba 8 mwaka 2012, yameonyesha kuwa Tanzania
bara kuna Watu milioni 43.6 na Zanzibar watu Milioni 1.3.
Rais
Jakaya Kikwete ndiye alitangaza matokeo hayo jana(Desemba 31) jijini Dar es
Salaam na kuwataka Watanzania kupunguza kasi ya kuzaliana.
![]() |
Ramani ya Tanzania. |
Akizungumza
katika viwanja vya Mnazi Mmoja wakati wa uzinduzi huo, Rais Kikwete ambaye
aliambatana na viongozi mbalimbali wa kitaifa, alisema kuwa matokeo hayo ni
ishara kwamba ifikapo mwaka 2016 kuna uwezekano wa idadi hiyo kufikia milioni
51 jambo ambalo linaweza kuwa ni mzigo kwa taifa, jamii na hata katika masuala
ya uchumi.
Rais
alifafanua kuwa jamii inapaswa kuyachukulia kwa uzito matokeo hayo hasa katika
masuala ya kupanga uzazi pamoja na kuongeza bidii ya kufanya kazi.
Rais
Kikwete alisema kuwa Watanzania wanapaswa kuongeza nguvu ya kufanya kazi zaidi
kwa kuwa idadi imekuwa kubwa na inaongezeka kwa kasi kubwa.
“Kupanga
uzazi ni jambo la msingi sana na tuzingatie hayo ili kuweza kupiga hatua maana
matokeo hayo yanaashiria idadi ya watu milioni 10 imeongezeka tangu sensa ya
mwaka 2002 kufanyika,” alisema.
Alisema
kuwa matokeo yatakayofuata yatatangazwa Februari ambapo yatatoa idadi ya
wanaume na wanawake na matokeo mengine kutolewa Aprili 2013.
![]() |
Rais Kikwete. |
Rais
aliongeza kuwa zoezi hilo linagharimu fedha nyingi lakini serikali inalazimika
kufanya kutokana na kutakiwa kupanga sera na mikakati ya maendeleo ambapo kwa
sensa ya mwaka 2012 imegharimu kiasi cha sh bilioni 140 na zilizotumika hadi
sasa ni sh bilioni 124.
“Hata
hivyo ninapongeza kukamilika kwa zoezi hili la awali kwani kulikuwa na
purukushani nyingi na maneno mengi ya kutaka kuvuruga…wapo walioendesha na
kuhamasisha wengine wasusie, wapo waliotaka kuendesha maandamano wakati wakijua
ni wakati wa sensa lakini pamoja na mitihani yote tumeweza kupata matokeo,”
alisema.
Alisema
sensa hiyo ni ya tano kufanyika tangu Muungano ambapo ya kwanza ilifanyika
mwaka 1967 na idadi ya watu ilikuwa milioni 12,313,469, bara wakiwa milioni
11,958,654 na visiwani 354,400.
Alisema
kuwa sensa ya kwanza ilifanyika mwaka 1910. Sensa nne za mwisho zilifanyika
baada ya Uhuru katika miaka ya 1967, 1978, 1988 na 2002.
Kulingana
na sensa ya mwisho iliyofanyika Agosti 2002, idadi ya watu nchini ilikuwa
34,443,603.
![]() |
Waziri
Mkuu
Mizengo
Pinda.
|
Naye
Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya sensa, alisema kuwa
mchakato huo ulikabiliwa na changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na watu wanne
kupoteza maisha huku wengine wakijeruhiwa.
Alisema
kuwa zaidi ya sh bilioni 90 zilitumika kuwalipa vijana walioajiriwa wakati wa
sensa ambapo vijana 200,000 waliajiriwa katika kuhesabu na 400 wakati wa
uchambuzi.
No comments:
Post a Comment