Nchi za Afrika mashariki kuhamia mfumo wa Digitali ifikapo Desemba 31 saa 6 Usiku ambapo kituo chochote kitakachokaidi agizo hilo kitachukuliwa hatua za kisheria. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, December 31, 2012

Nchi za Afrika mashariki kuhamia mfumo wa Digitali ifikapo Desemba 31 saa 6 Usiku ambapo kituo chochote kitakachokaidi agizo hilo kitachukuliwa hatua za kisheria.


TV ndogo ya analogia

na kubwa ya Digitali.

Nchi za Afrika mashariki zinatarajia kuhamia mfumo wa Digitali ifikapo Desemba 31, TCRA imevitaka Vituo vyote vya televisheni kuhamia digitali ifikapo tarehe hiyo ambapo kituo chochote kitakachokaidi agizo hilo kitachukuliwa hatua za kisheria.


 
Nchini Kenya kunahofiwa kutoingia katika mfumo huu hapo ifikikapo 31 Deseba 2012 baada ya Bodi ya Walaji nchini humo kuweka pingaimzi wakidai gharama za Ving’amuzi zipuguzwe kwa wananchi.



Kwa upande wa Tanzania mkakati huo bado haujakamilika mikoa yote, Mikoa ambayo haijaunganishwa ­ katika masafa ya Digitali haitaathirika na tatizo la matangazo ya analogia hapo Desemba 31 mwaka huu.



Upatikanaji wa Ving'amuzi umekuwa moja ya vikwazo ambavyo serikali za Afrika mashariki zinahitajika kuweka mkakati utakaorahisisha upatikanaji wa Ving’amuzi hivyo kwa watumiaji wote wa vyombo hivyo vya habari.



Wakiongea kwa nyakati tofauti baadhi ya wananchi wa Afrika mashariki wamezitaka mamlaka zinasohusika na mpango huo, kusogeza mbele tarehe ya kubadilisha mfumo wa analogia ili kutowanyima haki yao ya kupata habari na matangazo mengine muhimu.



Aidha uchunguzi  uliyofanywa  umebaini kwamba, Maduka mengi yanayouza Ving’amuzi yamegubikwa na idadi kubwa ya wateja ambao wengi wao hawajawa na elimu ya kutosha kuhusu mabadiliko yanayotarajiwa.



Kwa upande wao TRC wanasema mabadilko haya yatatoa unafuu kwa wakazi wa mikoa ambayo haijaungwa katika masafa ya Digitali, mkurugenzi wa mawasiliano TCRA Inocent Mongi amesema kuwa hawatazima mitambo ya analojia katika baadhi ya mikoa hiyo kutokana na sehemu hizo kuwa na uhitaji wa kufanya mabadiliko taratibu.



Bodi ya Walaji Nchini Kenya hivi karibuni imeifikisha Mahakamani Tume ya mawasiliano Nchini humo ikiitaka kusogezwa mbele kwa zoezi la kuzima matangazo ya analogia hapo Desemba 31 mwaka huu.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad