Mfaransa Patrick Liewig
Na waandishi wa Habari
kwenye Uwanja wa Ndege
wa Kimataifa wa Julius
Nyerere jijini Dar es Salaam.
|
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam, Liewig aliyekuja kutwaa nafasi iliyoachwa wazi na Mserbia Milovan Cirkovic, amesema 'Wanamsimbazi' watarajie mambo mazuri kutoka kwake, lakini kwa sharti la kumpa ushirikiano katika kila hatua wakati atakaposaini mkataba wa kuifundisha timu hiyo na kuanza kibarua chake.
Katibu wa Simba,
Evodius Mtawala
(kushoto)
akiongozana
na kocha mpya wa klabu
hiyo,
Patrcik Liewig
baada ya
kuwasili Uwanja wa
Ndege
wa Julius Nyerere,
Dar es
Salaam.
|
"Nimefurahishwa sana na mapokezi haya... najihisi kuwa nina deni kubwa.
Naamini nitapata ushirikiano wa kutosha na baada ya kuzoeana na wachezaji,
naamini Simba itafika mbali katika kila michuano," alisema kocha huyo.
Miongoni mwa watu waliofika uwanjani kumpokea kocha huyo ni Katibu Mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, ambaye aliwaongoza mamia ya mashabiki wa Simba kumpokea kwa maandamano ya magari na pikipiki za bodaboda na bajaji.
Taarifa kutoka ndani ya Simba zinaeleza kuwa kocha huyo atasaini mkataba wa kuifundisha klabu hiyo kwa miezi 18 na tukio hilo litakamilishwa kesho.
Wakati
kocha huyo akitua ,Kikosi cha Simba SC kiko huko Visiwani Zanzibar kushiriki
mashindano ya Kombe la Mapinduzi kwenye Uwanja wa Amaan visiwani
Zanzibar, kesho(Januari 2, 2013).
Kwa
mujibu wa Msemaji wa Kamati ya Mashindano, Farouk Karim, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya
Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ufunguzi huo unaotarajiwa kufanyika usiku na
kufuatiwa na mechi kati ya Simba ya Tanzania bara na Jamhuri ya Pemba.
Aidha
mchezo mwingine siku hiyo utakuwa kati ya Mtibwa Sugar dhidi ya
Miembeni, ambao utafanyika kwenye uwanja wa Mao Tsetung kuanzia saa 10 alasiri
na kwamba, maandalizi yote yamekamilika, ambapo timu zote shiriki zimeshaanza
kuwasili visiwani humo.
Karim
alisema kuwa, Januari 4 kutakuwa na mechi mbili, ambapo Jamhuri na Bandari
zitacheza saa 10 alasiri na saa 2 usiku, Tusker ya Kenya itakuwa dimbani dhidi
ya Simba huku Januari 5, Mtibwa Sugar itapepetana na Coastal Union saa 10
alasiri, wakati Miembeni na Azam shughuli itakuwa saa 2 usiku.
Alisema,
mechi nyingine zitakuwa kati ya Tusker na Jamhuri saa 10 alasiri na mechi ya
mwisho ya kundi hilo itakuwa kati ya Simba na Bandari wakati kundi B zitakuwa
kati ya Miembeni na Coastal Union saa 10 alasiri na mechi ya mwisho katika
mzunguko huo wa kwanza ni kati ya Azam na Mtibwa Sugar.
Karim
aliongeza kuwa, hatua ya nusu fainali itaanza Januari 9 kwa mchezo mmoja huku
wa pili ukiwa ni Januari 10, ambapo mechi zote zitapigwa saa 2 usiku.
Aliongeza
kuwa, fainali za michuano hiyo zitarindima Januari 12 saa 2 usiku, ikiwa ni
kilele cha michuano hiyo ambayo hufanyika kila mwaka.
No comments:
Post a Comment