Uganda wametwaa Taji lao la 13 la Ubingwa wa CECAFA huku Robert Ssentongo amepewa tuzo ya ufungaji bora wakati anazidiwa mabao na washambuliaji wa Tanzania Bara, John Raphael Bocco na Mrisho Khalfan Ngassa, ambao kila mmoja ana mabao matano. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, December 09, 2012

Uganda wametwaa Taji lao la 13 la Ubingwa wa CECAFA huku Robert Ssentongo amepewa tuzo ya ufungaji bora wakati anazidiwa mabao na washambuliaji wa Tanzania Bara, John Raphael Bocco na Mrisho Khalfan Ngassa, ambao kila mmoja ana mabao matano.

Uganda (The Cranes)
Kwenye  Fainali ya CECAFA TUSKER 2012 CHALENJI CUP,magoli mawili ya kujifunga kutoka kwa wachezaji wa timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, yamewapa wenyeji Uganda (The Cranes) ubingwa wa 13 wa michuano ya mataifa ya Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Chalenji) kufuatia ushindi wa 2-1 katika mechi ya fainali iliyochezwa kwenye Uwanja wa Mandela, Namboole, Kampala jana Desemba 08,2012.


Kwa kutwaa kombe hilo, ambalo ni la nne kwa kocha wao Bobby Williamson, Uganda imeondoka na zawadi ya kwanza ya kombe na dola 30,000 wakati Wakenya walioshina nafasi ya pili wamepata dola 20,000 huku Zanzibar Heroes iliyoshika nafasi ya tatu imepata dola 10,000.




Nahodha wa Uganda, Hassan Wasswa akiwa amenyanyua Kombe la Ubingwa wa CECAFA Tusker Challenge 2012 baada ya kuifunga Kenya kwenye Uwanja wa Mandela mjini Kampala, Uganda mabao 2-1 na kutwaa Kombe hilo kwa mara ya pili mfululizo.


Mrisho Ngassa
Nyota wa Uganda, Brian Umony ametwaa tuzo ya Mchezaji Bora wa Michuano hiyo na tuzo ya kipa bora imekwenda kwa kipa wa Uganda, Hamza Muwonge, ambaye ameruhusu goli moja tu katika michuano yote, ambapo Uganda wameshinda mechi zao zote.



Utata umekuja katika tuzo ya mfungaji bora baada ya kupewa Robert Ssentongo wa Uganda, mwenye magoli manne na kuachwa Mrisho Ngassa na John Bocco waliofunga magoli matano kila mmoja.



WAFUNGAJI CECAFA TUSKER CHALLENGE 2012.




John Bocco                   Tanzania 5

Mrisho Ngassa              Tanzania 5

Robert Ssentongo         Uganda   4

Brian Umony                 Uganda   3

Khamis Mcha                Zanzibar  3

Suleiman Ndikumana    Burundi   3 (1 penalti)

Chris Nduwarugira        Burundi   3

Geoffrey Kizito              Uganda   2

David Ochieng              Kenya      2

Clifton Miheso               Kenya      2

Dadi Birori                     Rwanda   2

Mike Barasa                  Kenya      2


 
Rais wa CECAFA, Leodegar Tenga alikuwapo jukwaani kuwakabidhi zawadi washindi.


Zanzibar Heroes
Zanzibar Heroes ilipata ushindi wa tatu baada ya kuwafunga ndugu zao wa Tanzania Bara kwa penalti 6-5, baada ya dakika 90 za mechi yao kumalizika kwa sare ya 1-1.

 

Tanzania Bara walihitaji kukaza kwa dakika nne tu za mwisho ili kupata ushindi wa 1-0 kupitia goli la mapema dakika ya 10 lililofungwa na Mwinyi Kazimoto kufuatia pasi ya kichwa ya John Bocco.



Lakini mchezaji Abdallah Othman Ali aliyeingia akitokea benchi kuchukua nafasi ya kiungo Suleyman Kassim 'Selembe', aliisawazishia Zanzibar goli katika dakika ya 86.
 


Kocha Mkuu wa Zanzibar, Salum Nassor Bausi akiwa amebebwa na wachezaji wake kwa furaha


Sabri Ali Makame ndiye aliyefunga penalti iliyowapa ushindi Zanzibar baada ya beki Kelvin Yondani kupiga nje penalti yake wakati wa kupigiana penalti moja-moja baada ya tano za kwanza kumalizika huku kila timu ikiwa imefunga nyingine moja-moja ya hatua hiyo ya "piga nikupige".



Katika penalti tano-tano za kwanza kila timu ilikosa penalti moja. Mwinyi Kazimoto alikosa penalti ya nne kwa upande wa Bara iliyodakwa na kipa wa Zanzibar wakati Nasoro Masoud "Chollo" alikosa penalti ya nne ya Zanzibar Heroes iliyodakwa na kipa wa Bara, Juma Kaseja.



Waliopata penalti zao kwa upande wa Bara walikuwa Erasto Nyoni, Amir Maftah, Shabani Nditi, Shomary Kapombe na Frank Domayo, wakati waliofunga kwa upande wa Zanzibar walikuwa ni Khamis Mcha,  Samih Nuhu, Aggrey Morris, Abdallah Othman Ali, Nadir Haroub 'Cannavaro', na Sabri Ali Makame aliyepiga ya ushindi.   


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad