Soma Utafiti Mbunge John Mnyika, Kabwe Zitto (CHADEMA) Godfrey Zambi (CCM) ndiye wanashikilia rekodi ya ukinara wa kuchangia huku Edward Lowassa, Zakia Meghji na Lameck Airo (CCM) ni miongoni mwa wabunge ambao wamechangia na kuuliza maswali machache Bungeni . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, December 31, 2012

Soma Utafiti Mbunge John Mnyika, Kabwe Zitto (CHADEMA) Godfrey Zambi (CCM) ndiye wanashikilia rekodi ya ukinara wa kuchangia huku Edward Lowassa, Zakia Meghji na Lameck Airo (CCM) ni miongoni mwa wabunge ambao wamechangia na kuuliza maswali machache Bungeni .


Mbunge wa Jimbo la Ubungo,

John Mnyika.

Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa, Zakia Meghji (mbunge wa kuteuliwa) na Lameck Airo (CCM) ni miongoni mwa wabunge ambao wamechangia na kuuliza maswali machache bungeni tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu 2010.



Kwa mujibu wa mtandao wa Bunge, Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA) ndiye anashikilia rekodi ya ukinara wa kuchangia akifuatiwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA) na Godfrey Zambi wa Mbozi Mashariki (CCM).



Utafiti huo ambao hauhusishi takwimu za mkutano wa Novemba haukuwajumuisha mawaziri, manaibu wao, Spika, naibu wake, wenyeviti watatu wa Bunge, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa vile nafasi zao zinawapa uwezekano mkubwa wa kuchangia hoja wakati wowote.



Katika rekodi hiyo, Mnyika ambaye hiki ni kipindi chake cha kwanza bungeni, amechangia mara 184, kuuliza maswali ya nyongeza 28 na ya msingi 7, Zitto amechangia 79, maswali ya nyongeza 25 na maswali ya msingi 8, huku Zambi akiwa amechangia mara 70, maswali ya nyongeza 26 na ya msingi 9.




Mbunge wa Kigoma Kaskazini,

Kabwe Zitto.
Kulingana na takwimu hizo, wabunge kumi waliochangia na kuuliza maswali mara chache ni Mwanakhamis Said Kassim (CCM), ambaye rekodi inaonesha hajawahi kuuliza swali la msingi wala nyongeza isipokuwa amechangia mara mbili tu.



Anayefuata ni Waziri Mkuu aliyejiuzulu mwaka 2008, Lowassa ambaye vile vile hajawahi kuuliza swali la msingi wala nyongeza bali kachangia hoja mara mbili.



Katika kundi hilo wamo Mbunge wa Rorya, Airo aliyechangia mara tatu, maswali ya msingi matatu, wakati Muhammed Amour Chombo (CCM) hajawahi kuuliza swali bali amechangia mara nne.



Muhammed Seif Khatib (CCM), hajawahi kuuliza swali bali amechangia mara tatu huku Ali Haji Juma (CCM), ameuliza swali moja la msingi, moja la nyongeza na kuchangia mara nne.




Mbunge wa Monduli,

Edward Lowassa.

Wamo pia Anna Maulida Komu (CHADEMA) na Shwawana Bukhati Hassan (CCM) ambao wamechangia mara tano bila kuuliza maswali wakati Meghji akiwa amechangia mara tisa bila kuuliza swali.



Rekodi hiyo pia inawaonesha Dk. Abdulla Juma Saadalla (CCM), Said Suleiman Said (CUF) na Salim Hassan Turky (CCM) waliochangia mara saba, na kuuliza swali la nyongeza moja.



Mbunge wa Gairo, Ahmed Shabiby (CCM), ndiye anafunga orodha hiyo akiwa amechangia mara tano na kuuliza swali moja la msingi na moja la nyongeza.



Katika kumi bora ya wabunge waliochangia mara nyingi, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA) anashika nafasi ya nne akiwa amechangia mara 93, ameuliza maswali ya nyongeza 19 na msingi 7, akifuatiwa na Diana Chilolo wa Viti Maalumu (CCM) aliyechangia mara 61, maswali ya nyongeza 41 na msingi 9.




Mbunge wa Kawe,

Halima Mdee.


Nafasi ya sita inashikiliwa na Halima Mdee wa Kawe (CHADEMA) akiwa na amechangia mara 59, maswali ya nyongeza 15 na ya msingi 6 akifuatiwa na Moses Machali wa Kasulu Mjini (NCCR-Mageuzi) mwenye michango 57, nyongeza 30 na maswali ya msingi 7.



Chritowaja Mtinda (CHADEMA) amechangia mara 53 na kuuliza maswali ya msingi 12 na nyongeza 19 akifuatiwa na Magdalena Sakaya (CUF) aliyechangia mara 52, maswali ya nyongeza 13 na ya msingi 4.



Mbunge wa Kisarawe, Seleman Jafo (CCM) alifuatia kwa michango 51, maswali ya nyongeza.


Habari na:http://www.freemedia.co.tz/daima/habari.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad