Kamanda
wa Polisi,
Mkoa
wa Kigoma
RPC.
Fraiser Kashai
|
Buyogera
amesema hayo wilayani Kasulu wakati wa mazishi ya Gasper Mussa Mkazi wa kijiji
cha Heru Shingi tarafa ya Makere wilayani Kasulu Mkoani Kigoma , aliyefariki dunia wakati wa
sikukuu ya Christmass kutokana na kipigo kutoka kwa askari polisi wilayani
humo.
Mbunge huyo
wa jimbo la Kasulu Vijijini amesema kuwa vitendo vya askari polisi wilayani
humo kuchukua hatua ya kuwapiga na kuua raia vimekuwa vikitokea mara kwa mara
na wameshatoa taarifa kwa jeshi la polisi lakini hakuna hatua zozote ambazo
zimeshachukuliwa hadi sasa.
Ili kuweka
mambo sawa mbunge huyo amelitaka jeshi la polisi kuwahamisha askari polisi
ambao wameakaa wilayani humo kwa muda mrefu kwani kukaa kwao kwa muda mrefu
kunawafanya wajione kama tayari wanamiliki uhai wa watu na kufanya chochote
wanchoweza.
Naye
Mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Herushingo, Babona Kihenge alisema kuwa
amesikitishwa na kitendo cha askari polisi kumpiga na kumuua mtuhumiwa jambo
ambalo linaondoa imani ya wananchi kwa jeshi hilo.
Babona
alisema kuwa vitendo vya polisi kuwapiga na kuwasababisha wananchi ulemavu wa
kudumu na wakati mwingine kusababisha vifo vimekuwa vikitokea mara nyingi na
kwa sasa wameiomba serikali kuchukua hatua kukomesha mauaji hayo yanayofanywa
na polisi.
Kwa upande
wake Mganga Mkuu wa wilaya Kasulu, Jonathan Bujiji amethibitisha kwamba
marehemu Gasper alifikishwa hospitalini hapo akiwa amekufa jambo ambalo
linathibitisha kwamba marehemu alifia kituo cha polisi kabla ya kufikishwa
hospitalini hapo.
Aidha baadhi
ya wananchi wamelaumu kitendo hicho cha polisi hao kumpiga na kumuua mtuhumiwa
huyo ambaye chanzo cha ugomvi kinaelezwa kuwa ni kunywa pombe na kukataa kulipa
katika kilabu cha pombe ambacho kinamilikiwa na askari aliyeongoza mauaji hayo
aliyejulikana kwa jina la Peter.
Inaelezwa
kuwa sababu ya marehemu kukataa kulipa pombe aliyokunywa kilisababishwa na
askari huyo kukaidi kumlipa pesa zake kama ujira wa kazi ya kukarabati baadhi
ya maeneo ya kilabu hicho cha pombe kabla sikukuu.
No comments:
Post a Comment