IBF Yampongeza Bondia Mtanzania Fransis Cheka kwa kuwa bingwa mpya wa uzito wa Super Middle katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki yaa Kati. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, December 28, 2012

IBF Yampongeza Bondia Mtanzania Fransis Cheka kwa kuwa bingwa mpya wa uzito wa Super Middle katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki yaa Kati.

Francis Cheka

Shirilisho la Ngumi la Kimataifa (IBF) limepongeza bingwa mpya wa uzito wa Super Middle katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki yaa Kati, Mtanzania Francis Cheka.



Katika barua yake aliyomtumia Francis Cheka ya tarehe 28/12/2012 Mwenyekiti wa kamati ya Ubingwa wa IBF/USBA Lindsey Tucker alisema “Tunachukua fursa hii kukutakia maisha na mafanikio mazuri kama bingwa wa IBF na kumhimiza kuishi kama bingwa”.


Cheka atatakiwa kutetea taji lake katika kipindi cha miezi sita kufikia mwezi wa 6 mwakani dhidi ya mpinzani ambaye ana rekodi ya mapambano yasiyopungua 15 na mengi awe ameyashinda hususan mapambano mawili ya mwisho.


Aidha Bondia Francis Cheka alimaliza mwaka vizuri baada ya kuibuka na ushindi wa pointi 80-75 dhidi ya bondia kutoka Malawi, Chiotra Chimwemwe katika pambano lao hilo kali la kimataifa la  uzito wa Super Middle katika bara la Afrika, Ghuba ya Uajemi na Mashariki yaa Kati lililofanyika kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha juzi.



Chimwemwe ambaye alitajwa kuwa ni mwanajeshi wa cheo cha luteni usu nchini kwao Malawi, alionyesha ushindani mkali lakini hadi kufikia raundi ya 12, ni Cheka ndiye aliyeibuka kidedea baada ya majaji kumpa ushindi wa pointi 80-75.



Matokeo hayo yalimfanya Cheka aendeleze vipigo kwa kila bondia aliyekutana naye na hivyo kumaliza vyema mapambano yake mwaka huu.



Akizungumza mara baada ya pambano hilo, Cheka alisema kuwa amefurahi kwani mpinzani wake alionyesha umahiri mkubwa.



 Chimwemwe alikubaliana na matokeo na kumpongeza Cheka

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad