Boxing Day football –Liverpool,Manchester City wakinyukwa huku Chelsea,Tottenham na Manchester United raha tupu katika Ligi kuu soka nchini Uingereza. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, December 27, 2012

Boxing Day football –Liverpool,Manchester City wakinyukwa huku Chelsea,Tottenham na Manchester United raha tupu katika Ligi kuu soka nchini Uingereza.



Liverpool
Timu ya Stoke City, ikiwa uwanja wa nyumbani wa Britannia, walizinduka toka kufungwa Bao la Penati la Sekunde 35 iliyofungwa na Nahodha Steven Gerrard na kuwatandika Liverpool bao  3-1.



Aidha magoli mbili ya wachezaji Jon Walters na la Kenwyne Jones ndio yamewapa Stoke City ushindi wao wa kwanza katika Mechi 4 na kuendeleza wimbi lao la kutofungwa katika Mechi 9 ikiwa na pamoja ya kutofungwa Uwanjani kwao tangu Februari Mwaka huu.



Kipigo cha Liverpool katika Dimba la  Britannia kimeendeleza Rekodi yao ya kutoshinda hapo na pia kuwarudisha hadi nafasi ya 10 wakiwa Pointi 8 nyuma ya Timu iliyokamata nafasi ya 4.



Manchester City
Nao Mabingwa watetezi  wa Ligi kuu soka Uingereza Manchester City ambao wako nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi hiyo , walijikuta wakichapwaa Bao 1-0 na Sunderland huko  uwanja wa Stadium of Light, kwa goli la Mchezaji wao wa zamani Adam Johnson na  hivyo kuwafanya wawe  Pointi 7 nyuma ya vinara Manchester United  ambao nao walijituma na kuwafunga Newcastle Bao 4-3   wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani wa  Old Trafford kwa Bao la ushindi kufungwa Dakika ya 90 na Chicharito huku Chelsea wakiitungua Norwich City kwa Bao 1-0 na kujizatiti nafasi ya 3 wakiwa Pointi 4 nyuma ya Manchester City huku wakiwa na Mechi 1 mkononi.



Gareth Bale
Aston Villa wakicheza na Tottenham wamekubali kulizwa bao 4-0 , ikiwemo Hetitriki ya Gareth Bale na kuwapa ushindi Tottenham  huo 4-0 dhidi ya Aston Villa waliokuwa kwao Villa Park na hicho kuwa kipigo chao cha pili kizito baada ya kutandikwa 8-0 na Chelsea majuzi.


MATOKEO: 


Jumatano 26 Desemba 2012 

Everton 2 Wigan 1

Fulham 1 Southampton 1

Man United
Man United 4 Newcastle 3

Norwich 0 Chelsea 1

QPR 1 West Brom 2

Reading 0 Swansea 0

Sunderland 1 Man City 2

Aston Villa 4 Tottenham 0

Stoke 3 Liverpool 1


MECHI ZIJAZO:
Jumamosi 29 Desemba 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana] 

Sunderland v Tottenham


[SAA 12 Jioni] 


Aston Villa v Wigan

Fulham v Swansea

Man United v West Brom

Norwich v Man City

Reading v West Ham

Stoke v Southampton


[SAA 2 na Nusu Usiku] 

Arsenal v Newcastle


Jumapili 30 Desemba 2012

[SAA 10 na Nusu Jioni] 

Everton v Chelsea


[SAA 1 Usiku] 

QPR v Liverpool


1Manchester United19  Point  46
2Manchester City19  Point  39
3Chelsea18  Point   35
4Tottenham19  Point   33
5Everton19  Point   33
6West Bromwich19  Point   33
7Arsenal18  Point   30
8Stoke19  Point   28
9Swansea City19  Point  25
10Liverpool19  Point  25
11Norwich City19  Point   25
12West Ham 18  Point  23
13Sunderland19  Point  22
14Fulham19  Point  21
15Newcastle 19  Point  20
16Aston Villa19  Point  18
17Southampton18  Point  16
18Wigan Athletic19  Point  15
19Reading19  Point  10
20QPR19  Point  10

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad