Chama Cha
Mapinduzi (CCM) jana kilikamilisha safu yake ya uongozi kwa kuwapitisha kwa
kishindo viongozi wa ngazi za juu wa Chama hicho katika uchaguzi ambao
ulionekana kuwa na nidhamu kutokana na kutokuwa na uharibifu wa kura.
Katika uchaguzi wa safu za juu za Chama hicho,
Mwenyekiti, Makamu wa Mwenyekiti Zanzibar na Bara wajumbe wa mkutano huo
walitekeleza ombi la Yusuph Makamba la kumchagua kwa kishindo Jakaya Kikwete
kuongoza CCM .
Anne Makinda |
Akitangaza
matokeo hayo Spika wa Bunge la Tanzania ambaye ndiye alikuwa msimamizi,Anne
Makinda alisema kwamba Mwenyekiti
alipata ushindi wa kura 2,395 sawa na asilimia 99.92 huku kura mbili
zikisema hapana.
Makamu
Mwenyekiti Zanzibar Dk Ali Shein alipata kura 2,397 wakati makamu wa Bara
Phillip Mangula naye alipata idadi hizo za kura huku kukiwa hakuna kura
zilizoharibika wala kusema hapana kwa viongozi hao wawili.
Mwenyekiti
wa CCM, Taifa, Jakaya Kikwete na Makamu wake wawili Rais wa Zanzibar, Dk. Ali
Mohamed Shein (Zanzibar) na Philip Mangula (Bara) wakiwa meza kuu baada ya
kutangazwa kushika nyandhifa zao.
|
Wajumbe
wakiserebuka baada ya Rais Jakaya Kikwete kutangazwa kuwa mshindi wa Uenyekiti
wa CCM, Taifa.
|
Mohamed Seif Khatib |
Mwenyekiti
wa CCM, Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuunda sekretarieti mpya baada ya
uchaguzi wa mwenyekiti na makamu mwenyekiti Bara na Zanzibar utakaofanyika leo.
Kwa
upande wa Zanzibar, matokeo hayo yanaonyesha kuwa walioshinda ni pamoja na
Mbunge wa Uzini, Mohamed Seif Khatib; Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk
Hussein Ali Mwinyi, Waziri wa Fedha Zanzibar, Omar Yussuf Mzee, Abdulhakim
Chasama na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la
Kujenga Taifa (JKT), Shamsi Vuai Nahodha.
Wengine ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais,
Samia Suluhu Hassan, Khadija Hassan Aboud, Bhaguanji Mansuria, Waziri wa
Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa na Khamis Mbeto.
Watu
maarufu walioangukia pua katika uchaguzi huo ni Naibu Waziri wa Ushirikiano wa
Afrika Mashariki, Dk Abdallah Juma Sadallah, mtoto wa Rais Mstaafu, Abdallah
Mwinyi ambaye pia ni Mbunge wa Afrika Mashariki, Mbunge wa Viti Maalumu, Kidawa
Salehe na Naibu Waziri wa Fedha wa zamani, Abdisalaam Issa Khatib.
Wajumbe
wakipiga kura.
|
Majina
ya wajumbe wa Nec walioshinda bara na kura walizopata katika mabano ni Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wassira aliyeongoza kundi
hilo kwa kupata kura 2,135, Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia,
January Makamba (2,093), Mwekahazina wa CCM, Mwigulu Nchemba (1,967), na Katibu
wa UVCCM, Martine Shigela (1,824).
Wengine
ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Uratibu na Bunge), William
Lukuvi (1,805), Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Kimataifa, Bernard Membe
(1,455), Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Mathayo David Mathayo (1,414),
Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Jackson Msome (1,207), Katibu Mkuu wa CCM, Wilson
Mukama (1,374) pamoja na Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Fenela Mukangara (984).
Wakati
walioshinda Bara na wapambe wao wakitambiana, majina makubwa yaliyoanguka
katika uchaguzi huo ni pamoja ni Mbunge wa Afrika Mashariki, Shy-Rose Bhanji,
Mbunge wa Nkenge, Assumpter Mshama, Richard Hiza Tambwe na Mbunge wa zamani wa
Muleba Kaskazini, Ruth Msafiri.
Mwenyekiti
Mstaafu wa CCM, Benjamin Mkapa akiongoza Mkutano Mkuu kwa muda baada ya Kikwete
kujiuzulu.
(Picha zote na Bashir Nkoromo)
|
No comments:
Post a Comment