Nao Mabingwa wa soka Africa ya
Mashariki na Kati Yanga SC imepata ushindi wa kwanza ndani ya mechi tatu za
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kuifunga JKT Ruvu mabao 4-1 kwenye
Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga walikuwa tayari mbele kwa
mabao 2-0, yaliyotiwa kimiani na Nahodha, Nadir Haroub Ally ‘Cannavaro’ dakika
ya nne na Didier Kavumbangu dakika ya 31, mabao yote yakitokana na kazi nzuri
ya kiungo mshambuliaji Simon Msuva.
Kipindi cha pili, Yanga walirudi
tena kwa kasi na kufanikiwa kupata bao la tatu dakika ya 52, mfungaji Simon
Msuva kabla ya Didier Kavumbangu kufunga la nne dakika ya 65.
![]() | |
|
JKT ilipata bao lake la kufutia
machozi dakika ya 68 mfungaji Credo Mwaipopo.
![]() | |
|
Kwenye Uwanja wa Uwanja wa Sheikh
Amri Abeid Arusha wenyeji JKT Oljoro wameifunga Polisi Morogoro bao 1-0, bao
pekee la Paul Ndonga dakika ya 13 na Uwanja wa Mkwakwani, Tanga wenyeji
Coastal Union wamelazimishwa sare ya bila kufungana na Toto Africans.
Pos.
|
Club
|
P
|
W
|
D
|
L
|
GF
|
GA
|
GD
|
Pts
|
|
1
|
Azam
FC
|
3
|
2
|
1
|
0
|
4
|
2
|
2
|
7
|
|
2
|
Simba
SC
|
2
|
2
|
0
|
0
|
5
|
0
|
5
|
6
|
|
3
|
Coastal Union SC
|
3
|
1
|
2
|
0
|
2
|
1
|
1
|
5
|
|
4
|
JKT Oljoro FC
|
3
|
1
|
2
|
0
|
2
|
1
|
1
|
5
|
|
5
|
Mtibwa Sugar FC
|
3
|
1
|
1
|
1
|
3
|
1
|
2
|
4
|
|
6
|
Young Africans SC
|
3
|
1
|
1
|
1
|
4
|
4
|
0
|
4
|
|
7
|
Ruvu Shooting Stars
|
2
|
1
|
0
|
1
|
3
|
3
|
0
|
3
|
|
8
|
Toto African
|
3
|
0
|
3
|
0
|
3
|
3
|
0
|
3
|
|
9
|
African Lyon FC
|
2
|
1
|
0
|
1
|
1
|
3
|
-2
|
3
|
|
10
|
JKT Ruvu Stars
|
3
|
1
|
0
|
2
|
3
|
7
|
-4
|
3
|
|
11
|
Tanzania Prisons
|
2
|
0
|
2
|
0
|
1
|
1
|
0
|
2
|
|
12
|
Kagera Sugar FC
|
2
|
0
|
1
|
1
|
0
|
1
|
-1
|
1
|
|
13
|
Polisi
Moro
|
3
|
0
|
1
|
2
|
0
|
2
|
-2
|
1
|
|
14
|
JKT
Mgambo
|
2
|
0
|
0
|
2
|
1
|
3
|
-2
|
0
|
![]() |
|
RATIBA Mechi zijazo: Septemba 23. Mgambo JKT v Kagera Sugar[Mkwakwani, Tanga] Simba v Ruvu Shootings [National Stadium, Dar Es Salaam] African Lyon v Tanzania Prisons [Azam Complex, Dar es Salaam] |
Aidha Mechi tano za Ligi Kuu ya Vodacom za Super Weekend katika mzunguko wa kwanza
zitakazooneshwa moja kwa moja na kituo cha televisheni cha Super Sport zitaanza
kati ya saa 1.30 jioni na saa 1 kamili usiku.Septemba 28 mwaka huu kutakuwa na mechi kati ya Azam na JKT Ruvu itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 1 kamili usiku.
Mechi ya Simba na Tanzania Prisons itakayochezwa Septemba 29 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam itaanza saa 11 kamili jioni.
Yanga na African Lyon zenyewe zitapambana Septemba 30 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kuanzia saa 11 kamili jioni wakati Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar zitaoneshana kazi Oktoba 1 mwaka huu Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam kuanzia saa 10.30 jioni.
Mechi ya mwisho katika Super Weekend itakuwa Oktoba 3 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ikiwakutanisha watani wa jadi Yanga na Simba, na itaanza kutimua vumbi saa 1 kamili usiku.
Huko Visiwani Zanzibar,Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Zanzibar, Super Falcon wameendelea kuboronga katika ligi hiyo licha ya kumtimua kocha wake wiki iliyopita, baada ya kuchapwa mabao 2-0 na Jamhuri ya Pemba, kwenye Uwanja wa Gombani, Pemba, wakati Bandari imeibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya KMKM uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Uwanja wa
Gombani, Falcon ambao wataiwakilisha Zanzibar katika Ligi ya Mabingwa Afrika
mwakani, walikubali kipigo cha tatu mfululizo katika ligi hiyo kwa mabao ya
Mfaume Shaaban na Abdallah Mohammed, hiyo ikiwa mechi ya nane kwa Super Falcon
kupoteza.
Bandari
iliyopanda Ligi Kuu msimu huu ilipata bao lake la kwanza dakika ya 37,
lililotiwa kimiani na Mussa Omar, kabla ya KMKM kusawazisha dakika ya 44,
mfungaji Mudrik Muhib na Bandari wakapata bao la ushindi dakika 76 kupitia kwa
Mohammed Abdallah.
Ligi hiyo
inatarajia kuendelea tena kesho kwa mechi mbili, kisiwani Pemba, Chipukizi
wakicheza na Duma Uwanja wa Gombani, huku kisiwani Unguja, Malindi wakicheza na
Mafunzo katika uwanja wa Amaan.












No comments:
Post a Comment