Yanga yalia 3-0 kwa Wakata miwa wa Mtibwa Huku Mnyama Mkali Simba akichekelea mbele ya Maafande wa JKT Ruvu katika Ligi kuu soka Vodacom Tanzania bara. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, September 20, 2012

Yanga yalia 3-0 kwa Wakata miwa wa Mtibwa Huku Mnyama Mkali Simba akichekelea mbele ya Maafande wa JKT Ruvu katika Ligi kuu soka Vodacom Tanzania bara.


Mabasi mawili ya kisasa ambayo yatakabidhiwa kwa Klabu za Simba na Yanga yakiwa yameegeshwa katika viwanja vya aofisi za Kampuni ya Bia Tanzania kabla hayajabandikwa nembo za Kilimanjaro Premium Lager na za klabu husika tayari kwa hafla ya makabidhiano Ijumaa TBL Ilala.



Ligi Kuu Vodacom septemba 19, 2012, imeendelea kwa Yanga kutandikwa bao 3-0 huko Morogoro mikononi mwa Mtibwa Sugar wakati Jijini Dar es Salaam Mabingwa watetezi  Simba wakiendeleza wimbi la ushindi kwa kuichapa JKT Ruvu bao 2-0.


Huko Morogoro, Mtibwa Sugar walipata ushindi wao wa 3-0 dhidi  ya Yanga kwa bao za Dickson Daudi, Dakika ya 11, na bao mbili za Juma Javu za Dakika za 45 na 77.



Dakika ya 90 Yanga wakapata penati lakini Hamis Kiiza akashindwa kufunga na mwamuzi akapuliz kipenga cha kuashiria mwisho wa mchezo.

 

Hii ni Mechi ya pili kwa Yanga na hadi sasa hawajaambua ushindi na walitoka sare 0-0 na Tanzania Prisons katika Mechi yao ya kwanza.

Nao mabingwa watetezi wa ligi hiyo ya Vodacom Tanzania bara Wekundu wa Msimbazi, Simba wakicheza bila ya mshambuliaji wao tegemeo Emmanuel Okwi kutolewa nje kwa kadi nyekundu kipindi cha kwanza cha mchezo, walipata  ushindi wa bao 2-0 dhidi ya Maafande wa JKT Ruvu kwa mabao ya kiungo Amri Kiemba aliyefunga bao la kwanza na Haruna Moshi Boban aliyepiga la pili.

Kufuatia matokeo hayo Simba inaendelea kukamata usukani mwa ligi kwa kukusanya pointi 6, magoli matano ya kufunga na wakiwa hawajuruhusu nyvu zao kuguswa.

Simba walishinda mechi ya kwanza ya ligi kwa 3 - 0 dhidi ya African Lyon.



Huko Mwanza, wenyeji Toto African walitoka sare 2-2 na Azam FC huku Toto wakisawazisha bao katika Dakika ya 90 mfungaji akiwa Maganga na Mussa Saidi  ili hali  magoli ya wana lamba lamba Azam FC yakifungwa na  Abdulhalim Homoud na Kipre Tchetche .



Tanzania Prisons ya Mbeya ikiwa nyumbani Sokoine wametoka  sare ya bao 1 - 1 na Coastal Union ya Tanga, Kagera Sugar wametoka sare tasa na JKT Oljoro, huku Ruvu Shooting wakiifunga Mgambo JKT 2-1.

Aidha Ratiba ya Ligi kuu Vodacom Tanzania bara itaendelea tena  kwa  Mechi zijazo:



Septemba 22 .


Yanga v JKT Ruvu    [National Stadium, Dar Es Salaam].

Azam v Mtibwa Sugar [Azam Complex, Dar es Salaam]

JKT Oljoro v Polisi Morogoro [Sheikh Amri Abeid, Arusha]

Coastal Union v Toto Africans [Mkwakwani, Tanga]

Septemba 23.

Mgambo JKT v Kagera Sugar[Mkwakwani, Tanga]

Simba Ruvu v Shootings [National Stadium, Dar Es Salaam]

African Lyon v Tanzania Prisons [Azam Complex, Dar es Salaam]

 
 



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad