Vumbi la michuano ya Ligi ya Mabingwa lianzaa rasmi leo na kesho kwa kuzikutanisha timu mbalimbali barani Ulaya. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Tuesday, September 18, 2012

Vumbi la michuano ya Ligi ya Mabingwa lianzaa rasmi leo na kesho kwa kuzikutanisha timu mbalimbali barani Ulaya.

Leo jumanne Septemba 18 ndio mwanzo rasmi wa Michuano ya hatua ya Makundi ya UEFA ya kusaka Klabu Bingwa Ulaya, UEFA CHAMPIONZ LIGI, na zitakuwepo Mechi 8 za Makundi A hadi D lakini, bila shaka, kati ya hizo, BIGI MECHI, ile Mechi ya Mvuto, ni ile itakayochezwa Uwanja wa Santiago Bernabeu kati ya Mabingwa wa Spain Real Madrid na Mabingwa wa England, Manchester City..


Ingawa amekiri ameshindwa kuwapa morali Wachezaji wake na kusababisha waanze vibaya kutetea Taji lao la La Liga, Kocha wa Real Madrid, Jose Mourinho, amesema hatabadilisha Kikosi chake ila atachezesha  Wachezaji bora wenye kiwango cha hali ya juu ili kusaka Taji la 10 la Ubingwa wa Ulaya ambao Mashabiki wao wanaliita ‘LA DECIMA’.


Mara baada ya kufungwa bao 1-0 na Sevilla kwenye Ligi hapo Jumamosi, Mourinho alisikika akilalamika hana Timu lakini jana akiongea na Wanahabari ametamba: “Soka ni kuhusu leo na kesho sio jana! Jana ni historia!”


“Nilishindwa kuwapa morali Wachezaji wangu na hivyo walikosa motisha ya kucheza kwa kiwango cha juu na hilo ni kosa langu! Lakini kucheza na Manchester City inatupa changamoto! ”


 Nae kocha Roberto Mancini, Meneja wa Manchester City ambayo Msimu uliopita ilishindwa kuvuka hatua ya Makundi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, amesema hawajajiwekea malengo yeyote kwenye Mashindano ya Ulaya Mwaka huu lakini anategemea Timu yake kutwaa Ubingwa wa Ulaya Siku za usoni.


 KUNDI D



REAL MADRID v MANCHESTER CITY.



Hazijakutana kabla

* Real itakuwa timu ya kwanza kushinda mechi 100 za Ligi ya Mabingwa kama watawafunga mabingwa wa England. Wanaokaribia rekodi hiyo ni Manchester United iliyoshinda mechi 98 na Barcelona  mechi 97.

* Real ina rekodi ya kutisha ya kufunga mabao 24 katika mechi sita zilizopita ilizocheza nyumbani katika Ligi ya Mabingwa. Pia wameshinda mechi 11 kati 12 walizocheza Bernabeu, wamefungwa na Barcelona pekee katika nusu fainali ya mwaka 2011.

* City ilichapa Villarreal 3-0 ugenini msimu uliopita, lakini haijashinda katika mechi tatu zilizopita dhidi ya timu za Hispania.

* City imeshinda mechi sita kati ya nane ilizocheza Ulaya, lakini ina rekodi mbaya ugenini wakiwa wameshinda mechi mbili kati ya tisa walizocheza ugenini.


Chelsea begins the defense of its Champions League title against Italian champion Juventus, with both sides leading their respective leagues after an impressive opening few weeks of the season.

John Terry and Ashley Cole (both ankle) have shaken off knocks that ruled them out of England encounters during the international break and will feature against the Bianconeri. Roberto Di Matteo should also welcome back Juan Mata following the Spaniard's absence from the 0-0 draw against QPR at the weekend.

Juventus will be without former Inter defender Lucio (ankle) who is set to miss the majority of the season.

Following his impressive goal contribution in the season thus far, Kwadwo Asamoah looks set to make the starting XI ahead of Sebastian Giovinco. Nicklas Bendtner will continue to wait on the sidelines following his loan move from Arsenal.

Former Manchester United midfielder Paul Pogba is yet to make his Juventus debut but could feature after being included in the Old Lady's squad.


KUNDI A.

PARIS ST GERMAIN v DYNAMO KIEV


 Matokeo baina yao zilipokutana 


Wamekutana mara 4, Ushindi: PSG mara 2, Dynamo 1, Sare 1
Zilivyokutana Ligi ya Mabingwa hatua ya makundi.

19/10/94 Dynamo Kiev 1-2 Paris St Germain
2/11/94 Paris St Germain 1-0 Dynamo Kiev
UEFA: robo fainali
 9/04/09 Paris St Germain 0-0 Dynamo Kiev
16/04/09 Dynamo Kiev 3-0 Paris St Germain 

* PSG, imerudi kwa mara ya kwanza katika Ligi ya Mabingwa baada ya kuwa nje kwa miaka nane, inarekodi nzuri nyumbani kwenye michezo ya Ulaya na haijafungwa katika mechi 19 zilizopita, imeshinda mechi nne na hajaruhusu bao katika mechi 13.


* PSG haijaruhusu bao lolote jijini Paris katika mechi tatu ilizocheza hapo dhidi ya timu za Ukraine. Mbali ya mechi mbili dhidi ya Dynamo, pia iliifunga Karpaty Lviv 2-0 kwenye Europa Ligi misimu miwili iliyopita.


* Dynamo, imerejea katika michuano hiyo baada ya kukosa kwa misimu miwili, imeshinda mechi zake zote ilizocheza ugenini katika hatua ya kufuzu kwa kuifunga Feyenoord 1-0, na Borussia Moenchengladbach 3-1. Pia wameshinda mechi sita kati ya 12 walizocheza ugenini katika michuano ya Ulaya.


* Dynamo imeshindwa kusonga mbele zaidi ya hatua ya makundi katika mara tisa ilizocheza hatua hiyo. Mara ya mwisho kufuzu kwa hatua ya16 ilikuwa ni msimu wa 1999-2000 walipomaliza nafasi ya pili katika kundi lake.


DYNAMO ZAGREB v PORTO.



Matokeo baina yao zilipokutana Zimekutana mara 6: Dinamo imeshinda mara 3, Porto (2), sare 1 Zilivyokutana Ligi ya Mabingwa.



1 3/10/62 Porto 2-1 Dinamo Zagreb
17/10/62 Dinamo Zagreb 0-0 Porto14/09/83 Dinamo Zagreb 2-1 Porto
28/09/83 Porto 0-1 Dinamo Zagreb 21/10/98 Porto 3-0 Croatia Zagreb
4/11/98 Croatia Zagreb 3 -1Porto

* Dinamo ilikuwa na wakati mgumu katika Ligi ya Mabingwa msimu uliopita, ilipofungwa mechi sita za hatua ya makundi na kuweka rekodi yakufungwa mabao 22, pamoja na kipigo chaa 6-2 kutoka kwa Real Madrid naa 7-1 nyumbani kwa Olympique Lyon.


* Dinamo imeanza msimu huu vizuri kwa kushinda mechi tatu za kufuzu na hawajafunga katika michezo sita, huku wakishinda mechi tano kwa idadi ya mabao 12 na kuruhusu mabao manne tu.


* Porto imeshinda mechi10 kati ya 15 ilizocheza ugenini michuano ya Ulaya, lakini wamefunga mechi nne kati ya tano za karibuni na kipigo cha karibu zaidi ni kile cha mabao 4-0 walichopata kutoka kwa Manchester City katika Europa Ligi msimu uliopita.


* Kama Porto watashinda utakuwa ni ushindi wao wa  150 katika michezo 317 waliocheza Ulaya.



KUNDI  B


OLYMPIAKOS PIRAEUS v SCHALKE 04 


Hazijawahi kukutana kabla.



* Olympiakos imefungwa mabao nane katika michezo 13 iliyopita ya Ligi ya Mabingwa na haijawai kufungwa zaidi ya bao moja katika mechi zake.


* Olympiakos ina rekodi nzuri nyumbani dhidi ya timu za Ujerumani katika kipindi cha miaka 10 iliyopita, imeshinda mechi nne na kufunga mabao 16 na kufungwa mabao matatu tu.


* Schalke ikifunga bao kwenye mchezo huo litakuwa ni goli lao la 50 kwenye Ligi ya Mabingwa katika michezo 34 iliyocheza hadi sasa.


* Schalke safari yao pekee ya Ugiriki waliishia kufungwa 2-0 na Panathinaikos katika Ligi ya Mabingwa msimu wa 2001-02.



MONTPELLIER v ARSENAL 



Hazijakutana kabla


* Montpellier, ni mabingwa Ufaransa ambao wamefuzu  michuano hiyo mara sita. Mafanikio yao makubwa ilikuwa msimu wa1990-91 wakati walipofuzu kwa robo fainali ya Kombe la Washindi na kutolewa na Manchester United.

* Montpellier haijashinda mechi yoyote ya Ulaya iliyocheza nyumbani, ushindi wao wa mara ya mwisho ulikuwa wa 5-0 dhidi ya Steaua Bucharest msimu wa 1990-91.

* Arsenal imefungwa mechi nane kati ya 11 iliyocheza ugenini katika Ligi ya Mabingwa, lakini haijawai kushindwa inapocheza ugenini dhidi ya timu za Ufaransa. Wameshinda mechi tano kati ya tisa, pamoja na mechi nne zilizopita iliyocheza dhidi ya Olympique Marseille.

* Arsenal imecheza Ligi ya Mabingwa kwa miaka 15 mfululizo. Mafanikio yao makubwa yalikuwa mwaka 2006 walicheza fainali na kufungwa na Barcelona 2-1.



KUNDI C


AC MILAN v ANDERLECHT 


Rekodi baina yao
Zimekutana mara nne: Milan imeshinda mara mbili, na kutoka sare mara 2.

 24/11/93 Anderlecht 0-0 AC Milan
30/03/94 AC Milan 0- 0Anderlecht17/10/06 Anderlecht 0-1 AC Milan
1/11/06 AC Milan 4-1 Anderlecht.

* Milan imeshinda mechi nne tu kati ya 14 ilizocheza nyumbani katika Ligi ya Mabingwa, lakini hawajaruhusu bao katikati michezi nne kati ya mitano iliyopita. Katika michezo10 iliyopita iliyocheza dhidi ya timu za Ubelgiji nyumbani na ugenini, wamefungwa mabao mawili tu.

* Milan ni timu ya tano kucheza mechi 150 za Ligi ya Mabingwa. Timu nyingine zilizofikia idadi hiyo ni  Manchester United, Real Madrid, Barcelona na Bayern Munich.

* Anderlecht ilicheza mara ya mwisho Ligi ya Mabingwa miaka sita iliyopita. Mara ya mwisho msimu 2006-07 walimaliza mechi za hatua ya makundi bila ya kushinda mechi yoyote.

* Anderlecht imefungwa mechi nne zilizopita ilizocheza dhidi ya timu za Italia na haijawahi kushindi ugenini katika michezo saba iliyopita.




MALAGA v ZENIT ST PETERSBURG


 Hazijakutana kabla



* Kufuzu kwa Malaga kucheza Ligi ya Mabingwa kunaifanya kuwa klabu ya 13 kutoka Hispania kucheza michuano hiyo. Mara mwisho kuonekana katika michezo ya Ulaya ilikuwa miaka 10 iliyopita katika Kombe la UEFA walipocheza hatua ya robo fainali. 

* Zenit imepoteza michezo yote mitatu iliyocheza dhid ya klabu za Hispania, mara ya mwisho walifungwa 3-0 na  Real Madrid katika Ligi ya Mabingwa miaka mitatu iliyopita. Wameshinda mechi moja kati ya saba walizocheza ugenini katika Ligi ya Mabingwa.




BORUSSIA DORTMUND v AJAX AMSTERDAM 


Zimekutana mara mbili na zote imeshinda Ajax


6/03/96 Borussia Dortmund 0-2 Ajax Amsterdam
20/3/96 Ajax Amsterdam 1-0 Borussia Dortmund

* Borussia, imetupwa katika kundi ngumu msimu huu, watakuwa na kazi kubwa ya kusahau yaliyowakuta msimu uliopita walipofungwa mechi nne kati ya sita na kumaliza mkiani mwa kundi.

* Borussia imeshinda mechi moja kati ya saba ilizocheza dhidi ya klabu za Uholanza na imeshindwa kushinda mechi tatu iliyocheza nyumbani dhidi ya timu hizo.

* Ajax imefungwa mechi mbili kati ya tisa ilizocheza dhidi ya klabu za Ujerumani. 

* Ajax haikufungwa michezo minne kati ya sita ya Ligi ya Mabingwa msimu uliopita, lakini walishindwa kufuzu kwa hatua 16 bora.




RATIBA:
[Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku, Bongo Taimu]
Jumanne Septemba 18.

GNK Dinamo - FC Porto

Paris Saint-Germain FC - FC Dynamo Kyiv

Montpellier Hérault SC - Arsenal FC

Olympiacos FC - FC Schalke 04

Málaga CF - FC Zenit St. Petersburg

AC Milan - RSC Anderlecht

Borussia Dortmund - AFC Ajax

Real Madrid CF - Manchester City FC


RATIBA:
[Mechi zote kuanza Saa 3 Dak 45 Usiku, Bongo Taimu]
Jumatano Septemba 19.

FC Shakhtar Donetsk - FC Nordsjælland

Chelsea FC - Juventus

LOSC Lille - FC BATE Borisov

FC Bayern München - Valencia CF

FC Barcelona - FC Spartak Moskva

Celtic FC - SL Benfica

Manchester United FC - Galatasaray A.S.

SC Braga - CFR 1907 Cluj


• UEFA Champions League’’

• 2011/12 Chelsea

• 2010/11 Barcelona

• 2009/10 Internazionale

• 2008/09 Barcelona

• 2007/08 Man. United

• 2006/07 Milan

• 2005/06 Barcelona

• 2004/05 Liverpool

• 2003/04 Porto

• 2002/03 Milan

• 2001/02 Real Madrid

• 2000/01 Bayern

• 1999/00 Real Madrid

• 1998/99 Man. United

• 1997/98 Real Madrid

• 1996/97 Dortmund

• 1995/96 Juventus

• 1994/95 Ajax

• 1993/94 Milan

• 1992/93 Marseille

• 1991/92 Barcelona

• 1990/91 Crvena zvezda

• 1989/90 Milan

• 1988/89 Milan

• 1987/88 PSV

• 1986/87 Porto

• 1985/86 Steaua

• 1984/85 Juventus

• 1983/84 Liverpool

• 1982/83 Hamburg

• 1981/82 Aston Villa

• 1980/81 Liverpool

• 1979/80 Nottm Forest

• 1978/79 Nottm Forest

• 1977/78 Liverpool

• 1976/77 Liverpool

• 1975/76 Bayern

• 1974/75 Bayern

• 1973/74 Bayern

• 1972/73 Ajax

• 1971/72 Ajax

• 1970/71 Ajax

• 1969/70 Feyenoord

• 1968/69 Milan

• 1967/68 Man. United

• 1966/67 Celtic

• 1965/66 Real Madrid

• 1964/65 Internazionale

• 1963/64 Internazionale

• 1962/63 Milan

• 1961/62 Benfica

• 1960/61 Benfica

• 1959/60 Real Madrid

• 1958/59 Real Madrid

• 1957/58 Real Madrid

• 1956/57 Real Madrid

• 1955/56 Real Madrid
……………………………………………………….

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad