Mabingwa wa Ulaya Chelsea, wakiwa nyumbani Stamford Bridge, waliumwaga uongozi wa bao 2-0 na kutoka sare ya 2-2 na Juventus lakini wenzao Manchester United waitandika Galatasaray ya Uturuki kwa bao 1-0 . - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Thursday, September 20, 2012

Mabingwa wa Ulaya Chelsea, wakiwa nyumbani Stamford Bridge, waliumwaga uongozi wa bao 2-0 na kutoka sare ya 2-2 na Juventus lakini wenzao Manchester United waitandika Galatasaray ya Uturuki kwa bao 1-0 .

Chelsea walishindwa kulinda uongozi wa bao 2-0  zilizofungwa na mchezaji wao Mbrazil Oscar na kuiruhusu Juventus ya Italia  kurudisha bao zote kwa magoli ya Arturo Vidal na Fabio Quagliarella na kufanya mchezo huo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya uishe kwa sare ya magoli 2-2.



 Juventus wangeweza kushinda Mechi hiyo pale Mirko Vucinic alipopiga nje na mpira wa Kiungo Claudio Marchisio kuokolewa na Kipa Cech.




MATOKEO:
Jumatano Septemba 19.

FC Shakhtar Donetsk 2 FC Nordsjælland 0

Chelsea FC 2 Juventus 2

LOSC Lille 1 FC BATE Borisov 3

FC Bayern München 2 Valencia CF 1

FC Barcelona 3 FC Spartak Moskva 2

Celtic FC 0 SL Benfica 0

Manchester United FC 1 Galatasaray A.S. 0

SC Braga 0 CFR 1907 Cluj 2


Katika mchezo wa Mabingwa wa Hispania Real Madrid CF dhidi ya wenzao wa Uingereza  Manchester City,bao la Dakika ya 90 la Cristiano Ronaldo limewapa ushindi Real Madrid wa bao 3-2 dhidi ya Manchester City baada ya kutoka nyuma mara mbili na kusawazisha huku bao la pili wakifungwa katika Dakika ya 85 kwa frikiki ya Kolarov iliyombabatiza Xabi Alonso na kumhadaa Kipa Casillas.



Kinyume na Mchezo ulivyokwenda wakiwa wamezidiwa sana na ni uhodari wa Kipa Joe Hart ndio uliwaweka hai, Man City walitangulia kufunga katika Dakika ya 68 kwa bao la Dzeko na Real kurudisha Dakika ya 76 kwa bao la Marcelo.


Mara baada ya Mechi hiyo ya kwanza ya Kundi D la UEFA CHAMPIONZ LIGI, Kipa wa Man City, Joe Hart, alitamka: “Huwezi kuwa bao 2-1 mbele zikiwa zimebaki Dakika 5 na kufungwa gemu. Tujilaumu wenyewe. Hatuwezi kuendelea kuzungumzia uzoefu. Tunao Wachezaji wazuri wanaochezea Timu zao za Taifa. Wanacheza gemu nyingi sana.”

Kauli hiyo ya Joe Hart imemfanya Roberto Mancini alipuke na kubatuka: “Kama kuna Mtu anaweza kuiponda Timu basi ni mimi na si Joe Hart. Joe Hart yeye abaki kuwa Kipa tu. Mie ndio Jaji na si Joe Hart!”


MATOKEO:
Jumatano Septemba 18.

GNK Dinamo Zagreb 0 FC Porto 2

Paris Saint-Germain FC 4 FC Dynamo Kyiv 1

Olympiacos FC 1 FC Schalke 2

Montpellier Hérault SC 1 Arsenal FC 2

Málaga CF 3 FC Zenit St Petersburg 0

AC Milan 0 RSC Anderlecht 0

Borussia Dortmund 1 AFC Ajax 0

Real Madrid CF 3 Manchester City 2


MECHI ZIJAZO:

Jumanne Oktoba 2.

Juventus - FC Shakhtar Donetsk

FC Nordsjælland - Chelsea FC

Valencia CF - LOSC Lille

FC BATE Borisov - FC Bayern München

SL Benfica - FC Barcelona

FC Spartak Moskva - Celtic FC

CFR 1907 Cluj - Manchester United FC

Galatasaray A.S. - SC Braga


Jumatano Oktoba 3

FC Dynamo Kyiv - GNK Dinamo

FC Porto - Paris Saint-Germain FC

FC Schalke 04 - Montpellier Hérault SC

Arsenal FC - Olympiacos FC

RSC Anderlecht - Málaga CF

FC Zenit St. Petersburg - AC Milan

Manchester City FC - Borussia Dortmund

AFC Ajax - Real Madrid CF



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad