Ndani ya Uwanja wa Taifa, Jijini Dar
es Salaam jioni ya leo , katika Mechi ya kuashiria kuanza rasmi Msimu mpya wa
Mwaka 2012/13, Mabingwa wa Tanzania Bara, Wekundu wa Msimbazi Simba, leo walitoka nyuma kwa bao 2-0
na kubeba Ngao ya Jamii kwa ushindi
wa bao 3-2 dhidi ya Azam FC huku bao
la ushindi likifungwa na Mwinyi
Kazimoto.
Azam, chini ya Kocha wao mpya Boris Bunjak aliechukua wadhifa huo baada ya kutimuliwa
Mwingereza Stewart Hall walitangulia
kwa bao mbili za John Bocco na Kipre
Tchetche hadi mapumziko.
Lakini Simba walizinduka Kipindi cha Pili na kupiga bao 3 kupitia Daniel Akuffo, kwa Penati, Emmanuel Okwi na
Mwinyi Kazimoto.
Katika Mechi ya mwisho kwa Azam na Simba kucheza, ingawa Simba
ilichezesha Kikosi B, Simba hiyo
iliibuka mshindi kwa bao 3 lakini kwenye Mechi kabla ya hiyo, kwenye michuano
ya Kagame Cup, Simba ndio ilipata
kilio kikubwa walipopigwa bao 3-1 na Azam
FC kwenye Robo Fainali ya Kombe hilo na kutupwa nje ya Mashindano hayo huku
bao zote hizo 3 zikifungwa na Mshambuliaji hatari John Bocco.
Kwa Mwaka huu, hii itakuwa mara ya 7
kwa Simba na Azam kucheza.
MECHI
Simba v Azam 2012
Mapinduzi
Cup: Azam 2-0 Simba
Ligi
Kuu: Simba 2-0 Azam
Urafiki
Cup: Simba 1 Azam 1, Simba 2 Azam 2 [Simba watwaa Kombe kwa Penati 3-1]
Kagame
Cup: Azam 3- 1 Simba
Super
8: Simba 3- 1 Azam
Mechi hii ya Ngao ya Jamii
itafuatiwa na kuanza rasmi kwa Ligi Kuu Vodacom Wikiendi hii kwa Timu zote 14
kujimwaga Viwanjani.
RATIBA=Mechi
za Ufunguzi.
Septemba
15
Simba v African Lyon [Uwanja wa
Taifa, Dar es Salaam]
Polisi Morogoro v Mtibwa Sugar
[Jamuhuri Morogoro]
Tanzania Prisons v Yanga Sokoine
Mbeya]
Mgambo JKT v Coastal Union
[Mkwakwani Tanga]
JKT Ruvu v Ruvu Shootings [Azam
Complex Dar es Salaam]
Kagera Sugar v Azam [Kaitaba Kagera]
Toto Africans V JKT Oljoro [CCM
Kirumba Mwanza]






No comments:
Post a Comment