Simba ni ushindi tuu katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara huku Liverpool yatandika 5, Man City, Everton zashinda, Arsenal hoi kwa the Bluzzz. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, September 29, 2012

Simba ni ushindi tuu katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara huku Liverpool yatandika 5, Man City, Everton zashinda, Arsenal hoi kwa the Bluzzz.


Simba SC: Juma Kaseja, Nassor Masoud ‘Chollo’, Amir Maftah, Shomari Kapombe, Juma Nyosso, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba/Salim Kinje, Ramadhan Chombo/Jonas Mkude, Christopher Edward/Daniel Akuffo, Felix Sunzu na mrisho Ngassa.



Wekundu wa Msimbazi Simba SC leo imeendeleza wimbi lake la ushindi katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, baada ya kuichapa Prisons ya Mbeya iliyorejea Ligi Kuu msimu huu mabao 2-1  katika mchezo wa ligi hiyo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Mabao ya Simba yalitiwa kimiani na Felix Mumba Sunzu na Mrisho Ngassa, ambaye hilo ni bao lake la kwanza katika Ligi Kuu ndani ya mechi nne na la pili jumla tangu ajiunge na timu hiyo katika mechi saba alizocheza, wakati la Prisons lilifungwa na Elias Maguri.


Kwa ushindi huo Simba sasa imefikisha pointi 12 na kurejea kileleni mwa Ligi Kuu  ikiizidi pointi mbili Azam FC yenye pointi 10  katika nafasi ya pili, ingawa timu zote zimecheza mechi nne.



Prisons: 18.David Abdallah, 03.Aziz Sibo, 05.Laurian Mpalile, 16.Lugano Mwangama (Nahodha), 15.David Mwantika, 13.Khalid Fupi, 07.Misango Magai, 12.Fred Chudu/22.Julius Kwaga, 14.Elias Maguri, 17.Peter Michael/Sino Augustino na 19.John Matei/11.Hamisi Ally.



Hadi mapumziko, timu hizo zilikuwa zikwishafungana bao 1-1, Prisons wakitangulia kupata bao dakika ya sita baada ya Maguri kuwatoka mabeki wa Simba kupiga shuti lililodunda na kumchanganya kipa na Nahodha wa Simba, Juma Kaseja na kutinga nyavuni.



Kipindi cha pili, Simba walirudi na moto na kuanza moja kwa moja kulishambulia mfululizo lango la Prisons na dakika ya 55 Ngassa akafunga kwa shuti dhaifu, ambalo kipa wa Prisons, David Abdallah alidaka lakini mpira ukamtoka na kuingia nyavuni.


Dakika ya 87 Amir Maftah alipewa kadi nyekundu kwa kumchezea rafu Khalid Fupi wa Prisons, hivyo ataukosa mchezo ujao dhidi ya Yanga Jumatano na hiyo ni nafasi kwa chipukizi Paul Ngalema.


Hiyo inakuwa kadi ya pili nyekundu kwa Simba ndani ya mechi nne, awali katika mechi ya pili dhidi ya JKT Ruvu, Emmanuel Okwi alilimwa kadi ya aina hiyo kwa kumpiga kiwiko Kessy Mapande na akafungiwa mechi tatu.


Simba sasa inarejea kambini kwake visiwani Zanzibar kuendelea na maandalizi ya mchezo wa Jumatano, wakati watani wao, Yanga walioweka kambi Changanyikeni, Dar es Salaam kesho watacheza na African Lyon Uwanja wa Taifa.


Aidha matokeo ya leo Ligi Kuu England



Chelsea leo imeshusha kipigo cha kwanza Msimu huu kwa Arsenal kwenye Ligi Kuu England baada ya kuwachapa Bao 2-1 na wao kuendelea kukaa juu kwenye Msimamo wa Ligi wakiwa na Pointi 16 kwa Mechi 6 huku bao zote za Chelsea zikifungwa kilaini kutoka frikiki.


SUNDERLAND 1 WIGAN ATHLETIC 0



Bao la 5 kwa Mchezaji wao mpya Steven Fletcher leo limewapa ushindi wa kwanza Sunderland Msimu huu walipoifunga Wigan bao 1-0.

Bao hilo lilikuja Dakika tatu baada ya Wigan kubaki Mtu 10 kufuatia Kadi Nyekundu kwa Mchezaji wao Jordi Gomez alietolewa kwa kumchezea rafu mbaya Danny Rose.

FULHAM 1 MANCHESTER CITY 2

Edin Dzeko, akitoka benchi katika Dakika ya 86, aliifungia Man City Bao la ushindi walipoifunga Fulham Uwanjani Craven Cottage kwa bao 2-1.

Fulham ndio walitangulia kwa bao la Penati ya Dakika ya 10 iliyopigwa na Petric na City kusawazisha Dakika ya 43 mfungaji akiwa Sergio Aguero.

EVERTON 3 SOUTHAMPTON 1

Everton walitoka nyuma kwa bao moja na kupata ushindi bao 3-1 huku bao zao mbili zikifungwa na Nikica Jelavic.

Bao la Southampton lilifungwa na Gaston Ramirez na jingine la Everton lilipachikwa na Leon Osman.

READING 2 NEWCASTLE UNITED 2

Demba BA leo ameiokoa Newcastle aliposawazisha bao Dakika 7 kabla mpira kwisha ambalo lililalamikiwa kuwa ni la mkono.

Demba Ba pia alifunga bao la kwanza kwa Newcastle na bao za Reading zilipachikwa na Hunt na Kebe.



NORWICH CITY 2 LIVERPOOL 5

Luis Suarez alipiga hetitriki na bao moja moja za Nuri Sahin na Steven Gerrad ziliwapa Liverpool ushindi wa bao 5-2.

Bao za Norwich zilifungwa na Steve Morison na Grant Holt


STOKE CITY 2 SWANSEA CITY 0

Straika Peter Crouch leo alipiga bao mbili na kuipa Timu yake Stoke City ushindi wa ba o 2-0 dhidi ya Swansea City.

Ratiba:Jumapili Septemba 30
[Saa 12 Jioni]

Aston Villa v West Bromwich Albion

Jumatatu Oktoba 1
[Saa 4 Usiku]

Queens Park Rangers v West Ham United


Kwa ratiba na matokeo ya Ligi nyinginezo za Hispania,Ujerumani na Italia tazama juu kulia kwenye blog hii.
  


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad