TARIME.
Serikali
imesema kuwa kamwe haiwezi kumtegemea
mwekezaji kwa kila kitu huku baadhi ya Mambo yanaweza kufanywa na
wanajamiii wenyewe katika sehemu huska.
Kauli
hiyo ya Serikali ilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Tarime Bw John Henjewele katika
hafla ya kukabidhi Madawati kwa baadhi ya shule zinazozunguka mgodi wa ABG
North Mara, Vifaa vya Shule kwa baadhi ya wanafunzi na baiskel ya Magurudumu
matatu kwa watu watatu wasiojiweza.
Alisema
kuwa pamoja na Misaada inayotolewa na Mgodi huo kwa Jamii lakini pia serikali
inashukuru Mahusiano Mazuri yaliyopo katika Mgodi huo wa ABG North Mara na
Jamii.
Aidha
Meneja mkuu wa Mgodi wa North Mara Bw
Gary Chapman,amesema Mgodi huo ni miongoni mwa Migodi Afrika ambayo imekuwa
ikiwekeza katika Jamii hasa katika suala la Elimu,Afya,Maji na Maendeleo katika
Jamii.
Amesema
Pamoja na kutotimiza mahitaji kwa shule za Sekondary kwa asilimia mia lakini
watajitahidi kushirikiana na Jamii jiyo katika kujiletea Maendeleo.
“Mgodi
huu ni moja ya Mgodi Afrika ambao unajitolea katika kusaidia Jamii hasa katika
Elimu,afya,maji na Masuala la Maendeleo,lakini pamoja na kutotimiza Mahitaji ya
Jamii kwa asilimia kubwa bado tutaendelea kushirikia na nao” alisema Bw Gary Chapman.
Awali
akisoma Risala kwa Mgeni Rasmi Mwalimu mkuu wa shule ya Msingi Nyangoto Bw
Ghati Keraryo amesema kuwa shule zote mbili za Nyangoto na Matare zina
jumla ya Madawati 202 kati ya 654 ambayo yanahitajika na kwamba bado shule hizo
zina upungufu wa Viti 46 na meza 18.
Mbali
na Msaada huo wa Madawati kwa shule hizo,Mwalimu Ghati Keraryo ameuomba Mgodi huo kuendelea kujenga Shule hizo kama
Mkataba ulivyoainisha kati ya Kijiji na
Mgodi.
Amesema
kwa niaba ya Walimu wa shule hizo wanapenda kutoa shukurani kwa Mgodi wa ABG
North Mara kwa kutambua Umuhimu wa Changamoto moja wapo zinazokabili shule hizo
ikizingatiwa kwamba shule hizo zipo karibu na Mgodi huo.
Uongozi wa Mgodi huo umetoa Madawati zaidi
ya 1000 kwa shule za Nyangoto na Matare zilizopo katika eneo la Nyamongo
wilayani Tarime Mkoani Mara huku Miradi yote Mitatu ya Elimu ambayo ni msaada
wa baiskeli na Madawati hayo vikigharimu kiasi cha shilingi milioni 188.









No comments:
Post a Comment