Chama cha
mapinduzi CCM wilayani Ngara mkoani Kagera kimepata viongozi wapya kufuatia
uchaguzi uliofanyika jana ambapo aliyekuwa mwenyekiti wake Bi Helena Adrian
ameshindwa kuitetea nafasi yake .
Msimamizi wa
uchaguzi huo Kaptein Mstaafu Daud Salum Kateme amemtangaza Bw Hudson Bagege
kuwa mshindi wa nafasi ya Uenyekiti baada ya kupata kura 489 dhidi ya 257 za Bi
Helena Adrian.
Aidha Bw
Issa Samma amechaguliwa kuwa mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM, NEC baada ya
kupata kura 664 dhidi ya 111 alizopata Bi Helena Adrian huku Bi Ernestina Mpinzile
akipata kura 6.
Katika
mkutano huo Bw Damian Godard
amechaguliwa kuwa katibu wa itikadi na uenzi wa CCM katika wilaya ya Ngara
baada ya kupata kura 83 na kuwahsinda Bw
Georgia Myonyera na Erick Niramachumu.
Wajumbe wa
mkutano mkuu wa taifa ni Bw Said Sudy,Bw Mkiza Byamungu, Bw Stanlasus Batakanwa, Bi Ninian
Bakari na Bw Rehema Ramadhan.
Aidha huko
Jijini Mwanza aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Bw Lawrence Masha ameshinda uchaguzi wa mjumbe
wa halmashauri kuu ya CCM, NEC
kuwakilisha wilaya ya Nyamagana jijini Mwnaza .
Bw Masha
amewashinda wapinzani wake, Bw Biku Kotecha na Bw James Bwire katika uchaguzi
wa mjumbe wa NEC uliofanyika jana.
Katika
uchaguzi huo Kada wa siku nyingi wa CCM, Bw Raphael Shilatu amewashinda Bw
Yahya Nyaonge, Bw Joseph Bupamba na Bw Mashaka Kaguna.





No comments:
Post a Comment