Hivi ndiyo hali halisi ya ajali ya basi la Adventure lilipoteketea kwa moto wilayani Biharamulo mkoani Kagera huku Watu 63 wakinusurika kufa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, October 01, 2012

Hivi ndiyo hali halisi ya ajali ya basi la Adventure lilipoteketea kwa moto wilayani Biharamulo mkoani Kagera huku Watu 63 wakinusurika kufa.


Basi la Adventure likiwa na mizigo  ndani ya buti ikiteketea na moto.



Watu 63 wamenusurika kufa baada ya gari walilokuwa wakisafiria kutoka jijini Mwanza kwenda mkoani Kigoma, kuwaka moto.


Tukio hilo limetokea leo majira ya saa nne na nusu asubuhi katika kijiji cha Nyantakala wilayani Biharamuro, Mkoani Kagera, likihusisha gari aina ya Scania lenye namba T 928 AVP, mali ya Kampuni ya Adventure ya jijini Mwanza.



Juu ni mwonekano wa basi la adventure baada ya kuungua huku picha ya chini baadhi ya wananchi wakipakua badhi ya mizigo ambayo imesalia ndani ya basi hilo.



Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana kutoka wilayani Biharamuro, watu 8 kati yao wamejeruhiwa kwa moto na wamepelekwa katika hospitali ya wilaya ya Bukombe mkoani Geita, kwa matibabu zaidi.


Chanzo ajali hiyo ni hitilafu ya umeme iliyotokea katika betri ya Gari hilo ambapo hadi  sasa gharama halisi ya mali za abiria zilizoteketea kwa moto bado haijajulikana.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad