Fahamu matokeo ya mechi za Ligi kuu soka Uingereza,Hispania.Ujerumani na Italia Septemba 15 na 16 mwaka huu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Monday, September 17, 2012

Fahamu matokeo ya mechi za Ligi kuu soka Uingereza,Hispania.Ujerumani na Italia Septemba 15 na 16 mwaka huu.


Mara baada ya kuibandika Southampton bao 6-1 kwenye Mechi ya Ligi Kuu Uingereza hapo jana Uwanjani Emirates, Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, ameonyesha imani yake kuwa Kikosi chake kinaweza kutwaa Ubingwa.




Wenger ametamka: “Tunayo nafasi ya kutwaa Ubingwa lakini kwanza inabidi tuendeleze wimbi hili la ushindi. Tunao Wachezaji wazuri na inabidi waonyeshe ari ya ushindi.”


Arsenal, ambao mara ya mwisho kutwaa Ubingwa ilikuwa Mwaka 2004, wako Pointi 2 nyuma ya vinara Chelsea baada ya kucheza Mechi 4 na kutofungwa hata moja huku wakiwa wameruhusu bao moja tu la kufungwa.


MECHI ZINAZOFUATA:

-Jumanne Septemba 18=Montpellier v Arsenal [UEFA CHAMPIONZ LIGI]
-Jumapili September 23=Man City v Arsenal [LIGI KUU ENGLAND]
-Jumatano Septemba 26=Arsenal v Coventry [CAPITAL ONE CUP]
-Jumamosi Septemba 29=Arsenal v Chelsea [LIGI KUU ENGLAND]
-Jumatano Oktoba 3=Arsenal v Olympiakos [UEFA CHAMPIONZ LIGI]

Kocha Andre Villas-Boas leo ameambua ushindi wake wa kwanza wa Ligi Kuu England kama Meneja wa Tottenham walipoifunga Timu iliyopanda Daraja Msimu huu Reading bao 3-1 katika Uwanja wa Madejski.


Huku Watu wakianza kuhoji utawala wake ndani ya Tottenham baada ya Mechi 3 za Ligi bila ushindi, leo Timu ya Andre Villas-Boas ilicheza kwa kujiamini na kutawala hasa Viungo wao Mousa Dembele na Sandro huku Straika wao Jermaine Defoe akipiga bao mbili na jingine kufungwa na Gareth Bale.
 


MATOKEO:Jumamosi Septemba 15.

Norwich City 0 West Ham United 0
Arsenal 6 Southampton 1
Aston Villa 2 Swansea City 0
Fulham 3 West Bromwich Albion 0
Manchester United 4 Wigan Athletic 0
Queens Park Rangers 0 Chelsea 0
Stoke City 1 Manchester City 1
Sunderland 1 Liverpool 1


MSIMAMO  wa Timu za Juu:

[Kila Timu imecheza Mechi 4]

1 Chelsea  Pointi 10 

2 Man Utd  Pointi 9 

3 Arsenal  Pointi  8 

4 Man City  Pointi  8 

5 Swansea  Pointi  6 
======================


Mabingwa watetezi wa LA LIGA Hispania , Real Madrid, jana walifungwa 1-0 na Sevilla kwa bao lililofungwa katika Dakika ya Pili tu ya mchezo na Piotr Trochowski lakini Mahasimu wao, FC Barcelona, wameendeleza mwendo mzuri kwa kuinyuka Getafe bao 4-1.

Real Madrid, wakicheza ugenini, walitibuliwa na bao hilo la mapema na juhudi zao zote zilijaa papara na wakashindwa kurudisha licha ya kosa kosa nyingi.

FC Barcelona, ambao pia walikuwa ugenini, walipiga bao zao kupitia Adriano, Lionel Messi, bao mbili na moja ni Penati, na bao la 4 kufungwa na David Villa huku bao pekee la Getafe lilikuwa la kujifunga wenyewe ambalo Mascherano alijifunga.


Hadi sasa baada ya Mechi 4, Barca wako kileleni wakiwa na Pointi 12 na Real wapo nafasi ya 10 wakiwa na Pointi 4 tu.


Jumanne Usiku, Real Madrid watajikita kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI kucheza Mechi yao ya kwanza ya Kundi lao dhidi ya Manchester City Uwanjani Santiago Bernabeu na Barcelona watakuwa Nou Camp Jumatano kucheza na FC Spartak Moskva.


Mabingwa wa Italia, Juventus, leo wakicheza ugenini walitoka nyuma kwa bao 1-0 na kuitandika Genoa bao 3-1 katika Mechi ya Ligi Serie A wakiendeleza wimbi lao la ushindi katika Mechi zao zote 3 za Ligi Msimu huu na hizo ni salamu tosha kwa Mabingwa wa Ulaya Chelsea ambao watapambana nao Stamford Bridge hapo Jumatano katika Mechi yao ya kwanza ya Kundi E ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.


Na Vigogo AC Milan walipata mshituko baada ya kufungwa wakiwa nyumbani kwao bao 1-0 na Atalanta.



Jumamosi Septemba 15.

Palermo 1 Cagliari 1

AC Milan 0 Atalanta Bergamo 1

Jumapili Septemba 16.

Chievo Verona 1 Lazio 3
AS Roma 2 Bologna 3

Fiorentina 2 Catania 0

Genoa 1 Juventus 3

Napoli 3 Parma 1

Pescara 2 Sampdoria 3

Siena 2 Udinese 2

Torino 0  Inter Milan 2


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad