Huko Kaitaba, Mkoani Kagera, Timu iliyoshika nafasi ya Pili Msimu uliopita, Azam FC, iliidunga Kagera Sugar bao 1-0 kwa bao la Abdulahalim Humoud la Dakika ya 57.
![]() |
| Yanga, ambao walikuwa nafasi ya 3, Msimu uliopita wwalitoka sare huko Mbeya Uwanja wa Sokoine ya 0-0 na Tanzania Prisons. |
MATOKEO-Septemba 15.
Simba 3 African Lyon 0
Polisi Morogoro 0 Mtibwa Sugar Sugar 0
Tanzania Prisons 0 Yanga 0
Mgambo 0 Coastal Union 1
JKT Ruvu 2 Ruvu Shootings 1
Kagera Sugar 0 Azam 1
Toto Africans 1 JKT Oljoro 1
Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom
kuwania ubingwa wa Tanzania Bara kati ya Simba na African Lyon iliyochezwa jana
(Septemba 15 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 67,793,000.
Washabiki 11,505 walikata
tiketi kushuhudia mechi hiyo ambapo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000,
sh. 15,000 na sh. 20,000. Kila timu ilipata sh. 14,603,263.47 wakati asilimia
18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyokatwa ni sh. 10,341,305.08.
Mgawo mwingine umekwenda kwa
msimamizi wa kituo sh. 20,000, posho ya kamishna wa mechi sh. 114,000, mwamuzi
wa akiba sh. 70,000, et iti.sh. 3,175,000, vishina kwenye tiketi (attachments)
sh. 345,150, maandalizi ya uwanja (pitch preparation) sh. 400,000 na Wachina
(stadium technical support) sh. 2,000,000.
Umeme sh. 300,000, ulinzi na
usafi uwanjani sh. 2,350,000, Kamati ya Ligi sh. 4,867,754.49, Mfuko wa
Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,920,652.69, uwanja sh. 4,867,754.49,
Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,947,101.86, gharama
za mchezo sh. 4,867,754.49.
Nayo mechi ya ligi hiyo kati
ya Tanzania Prisons na Yanga iliyochezwa jana (Septemba 15 mwaka huu) Uwanja wa
Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya imeingiza sh. 50,435,000.
Aidha watazamaji 112 ndiyo
waliokata tiketi kushuhudia mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom kati ya JKT Ruvu na
Ruvu Shooting iliyofanyika jana (Septemba 15 mwaka huu) Uwanja wa Azam Complex,
Dar es Salaam.
Mapato yaliyopatikana katika
mechi hiyo ambapo viingilio vilikuwa sh. 3,000 na sh. 10,000 ni 340,000. Mgawo
ulikuwa kama ifuatavyo; kila timu sh. 29,465.87, asilimia 18 ya Kodi ya
Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 51,864.40, maandalizi ya uwanja sh. 100,000 na
tiketi sh. 89,916.
Kamati ya Ligi sh. 9,821.95,
Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 5,893.17, Chama cha Mpira wa
Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 3,928.78, gharama za mchezo sh. 9,821.95
na uwanja sh. 9,821.95.
Huko nako katika Ligi Kuu ya
Zanzibar maarufu Zanzibar Grand Malt Premier League imeendelea katika Viwanja viwili tofauti ambapo Kisiwani
Unguja, Klabu ya Bandari walicheza na Mafunzo na mechi hiyo imemalizika kwa
sare ya kufungana bao 1-1.
Katika muendelezo wa ligi hiyi hiyo
huko Kisiwani Pemba Klabu ya Jamhuri ambao ni Wawakilishi wa Zanzibar katika
michuano ya Kimataifa wakiwa na tiketi ya kushiriki katika Kombe la Shirikisho
walicheza na Chipukizi na kuanza kuonja machungu ya ligi baada ya kukubali
kipigo cha bao 3-0.
Mabao ya Chipukizi yalifungwa na
Muhsin Mohammed katika dakika ya 11 ya kipndi cha kwanza, bao la pili
likifungwa na Faki Maalim katika dakika ya 21 ya kipindi cha kwanza na mpaka
mapumziko Chipukizi walikuwa wakiongoza kwa mabao 2-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa
Jamhuri kutaka kusawazisha, huku Chipukizi wakitaka kuongeza, alikuwa ni Faki
Maalim kwa mara nyengine tena aliyeifungia Chipukizi bao la 3 katika dakika ya
60, na hadi dakika 90 zinamalizika za mchezo huo, Chipukizi 3 Jamhuri 0.
Ligi hiyo inatarajia kuendelea tena
kesho kwa mechi moja katika uwanja wa Amaan kwa kuzikutanisha timu za Mtende
Rangers na Chuoni.
Mtende v Chuoni [Amaan, Unguja]
Jumanne Septemba 18
Zimamoto v Mundu [Amaan, Unguja]
Jumamosi Septemba 22
KMKM v Bandari [Amaan, Unguja]
Super Falcon v Jamhuri [Gombani,
Pemba]
Jumapili Septemba 23
Mafunzo v Malindi [Amaan, Unguja]
Chipukizi v Duma [Gombani, Pemba]
Jumatatu Septemba 24
Mtende v Mundu [Amaan, Unguja]
Jumanne Septemba 25
Zimamoto v Chuoni [Amaan, Unguja]
TIMU 12 ZINAZOSHIRIKI:
TOKA UNGUJA:
-Bandari
-Chuoni
![]() |
TOKA PEMBA:
-Chipukizi
-Duma
-Jamhuri
-Super Falcon
|
-KMKM
-Mafunzo
-Malindi
-Mundu
-Mtende
Zimamoto












No comments:
Post a Comment