Wakati Rais Jakaya Mrisho Kikwete amemuita ikulu mwanamuziki Bongo Fleva, Nasibu Abdul Jumaa haya ndiyo Mambo 10 usiyoyajua kuhusu ‘Diamond Platnumz’. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, August 26, 2012

Wakati Rais Jakaya Mrisho Kikwete amemuita ikulu mwanamuziki Bongo Fleva, Nasibu Abdul Jumaa haya ndiyo Mambo 10 usiyoyajua kuhusu ‘Diamond Platnumz’.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amemuita ikulu mwanamuziki anayefanya vizuri kwa sasa kwenye Bongo Fleva, Nasibu Abdul Jumaa ‘Diamond Platnumz’ na kumpa jukumu maalum.


Kwa mujibu wa Diamond, Rais Kikwete  alimwita ikulu Magogoni, Dar es Salaam na kumpa shavu la kwenda kufanya shoo kwenye mkutano maalum utakaofanyika Washington DC nchini Marekani hivi karibuni.
 
“Yaa, rais aliniita akaniambia kuna shoo natakiwa kwenda kufanya Marekani.


“Kwa mara ya kwanza nitasafiri nje ya nchi na madensa wangu wanne na msemaji mmoja. Sasa hivi hawataki kutembea na kupanda magari wasije wakakosa hiyo safari,” alisema Diamond na kuongeza kuwa baada ya kuumwa, mawazo aliyaweka kwenye mchongo huo hivyo mambo mengine yataendelea ikiwa ni pamoja na kufanya kolabo na mwanamuziki wa kimataifa wa Nigeria, J. Martins.


Aidha kupitia Show ya Mkasi ya wiki  imetufanya tufahamu mambo 10 muhimu tusiyoyajua kutoka kwa Diamond kama ifuatavyo:


1. Yupo kwenye mazungumzo na label moja kubwa duniani ambao walimtafuta baada ya kufanya show ya Big Brother Africa.


2.Ana simu nne na moja ina line mbili, hivyo ana line tano.Simu yake huiweka silent muda wote kwakuwa zinapigwa muda mwingi. Anayo moja maalum ambayo watu wengi hawaijui.


3. Ana nyimbo 133 ambazo ameshazirekodi tayari.


4.Mama yake alikuwa anampeleka kwenye talent show na kumsubiria hadi usiku mpaka aperform ndo wanarudi wote. Ndugu zake wengine waliona anamdekeza mwanae.


5.Zamani alikuwa anapenda kurap lakini aliona ukirap huwezi kupata mademu. Alipokuwa akiimba watu wengi walikuwa wanamkataza kwakuwa waliona hawezi.


6. Q Chilla ndiye msanii anayempenda zaidi na muda mwingi husikiliza nyimbo zake.


7. Anamaliza mjengo wake uliopo Tegeta Dar es Salaam.


8.Anapenda kuja kuwa kama Usher Raymond.


9.Anapenda jinsi Dully anawasupport wasanii wachanga kwa kuwashauri na kuwapa moyo kuliko wasanii wengine wakongwe ndo maana anasema huwa hachuji.


10.Maproducer anaowazimia Tanzania Manecky, KGT, Manwalter na Marco Chali.



No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad