 |
Mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Kagame CUP ,
Yanga Tanzania wamekutana na Rais Paul
Kagame huko Mjini Kigali, Rwanda ambako leo wataanza Ziara yao rasmi ya Mechi
za Kirafiki kwa kucheza na Rayon Sports kwenye Uwanja wa Amahoro.
|
 |
Yanga ambao wametwaa Kagame CUP mara mbili mfululizo ambapo Mwenyekiti Yussuf
Manji, akiongea mbele ya Rais Kagame, alisema: “Tupo hapa kutoa shukran na
tukitambua mchango mkubwa wa Rais Kagame katika kuendeleza Michezo ambacho ni
kitu kinachotuunganisha Watu katika eneo hili!”
|
 |
Wachezaji wa Yanga wakisikiliza kwa makini
risala ya mwenyekiti wao.
|
Kwa upande wake Rais Kagame ametaka Udhamini
wake wa Mashindano ya Kagame Cup uendelee hata kama akistaafu kutoka kwenye
siasa.
Rais Kagame alisema: “Si kwa sababu
Rwanda ni tajiri ndio maana tumetoa udhamini bali ni alama ya kuimarisha
mchango wa michezo na umoja wa Watu wa eneo hili.”
 |
| Paul Kagame na Wachezaji wa Yanga |
Rais Kagame wa Rwanda alianza kudhamini
Mashindano ya Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati tangu Mwaka 2002
akitoa Dola 60,000 kama zawadi kwa Washindi na Dola 15,000 kama mchango wa
kuendesha michuano hiyo na ndio maana Kombi hilo huitwa rasmi Kagame Cup.
 |
Raisi wa Rwanda Paul Kagame
akisalimiana na Mama Fatma Karume na Kocha
wa Yanga Saintfield nchini Rwanda.
|
 |
Aidha Yanga ikiwa na Wachezaji wawili wa Amavubi, Timu ya
Taifa ya Rwanda, Haruna Niyonzima na Mbuyu Twite, itaondoka Kigali Jumatatu
kurejea Dar es Salaam.
|
No comments:
Post a Comment