Bw Said Sudi. |
Akitangaza
matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika jana katika ukumbi wa shule ya Sekondari
Ngara ,msimamizi wake Bw Wilbad Bambara amesema Bw.Soud amepata kura 241 kati
ya kura 259 zilizopigwa.
Bw
Bambara amesema mgombea mwingine Bw Allan Mnanga amepata kura 14 .
Aidha
Bw Bambara amewataja wajumbe 3 wa mkutano mkuu wa taifa wa jumuiya ya wazazi
waliochaguliwa kuwa ni Bw Mungele Kafiriti, Bi Elida Mhimbiza na Philimon Mpanju.
Akizungumza
mara baada ya Kuchaguliwa Bw.Sudi amewataka wana Jumuiya hiyo kushimamana na
kushirikiana kuiweka na kuijenga jumuiya ya wazazi wilaya ya Ngara ikae katika
madhumuni ya kuanzishwa kwake.
|
No comments:
Post a Comment