Barcelona 3 Real Madrid 2 katika kombe la SUPERCOPA Hispania. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, August 24, 2012

Barcelona 3 Real Madrid 2 katika kombe la SUPERCOPA Hispania.


Cristiano Ronaldo Dos Santos Aveiro

FC Barcelona imewafunge Mahasimu wao wakubwa katika soka huko Hispania Real Madrid  kwa Bao 3-2 katika Mechi ya kwanza ya kugombea kombe la Supercopa iliyochezwa Nou Camp Alhamisi Usiku, na kuifanya Mechi ya marudio ya kugombea Kombe hili itakayochezwa Jumatano ijayo Agosti 29 iwe Mechi inayosubiriwa kwa hamu kubwa na Wadau wa Soka Duniani kote.


Hii ilikuwa ‘El Clasico’ ya kwanza kwa Meneja mpya wa Barca, Tito Vilanova, na ametoka mbabe lakini bila shaka ipo kazi kubwa katika Mechi ya maruduano.


Hadi mapumziko bao zilikuwa 0-0 na ndipo mchezaji Ronaldo ndie aliefunga bao la kwanza kwa Real Madrid kwa kichwa kufuatia kona ya Ozil lakini Barcelona walisawazisha Dakika moja baadae kwa bao la Pedro ambae alipokea ndefu kutoka kwa Mascherano mara tu baada ya mpira kuwekwa kati baada ya Barca kufungwa.

Ronaldo

Lionel Messi

Bao la pili la Barcelona lilifungwa kwa Penati ya Lionel Messi baada ya Iniesta kuangushwa na Ramos ndani ya boksi na Barca wakapiga bao la 3 kupitia Xavi.


Lakini zikiwa zimesalia Dakika 5 mpira kwisha Kipa wa Barcelona Valdes alifanya makosa makubwa pale aliporudishiwa mpira na kujaribu utaalam wa kumzunguka Angel Di Maria lakini Mchezaji huyo wa Real Madrid akaunasa mpira na kufunga.

Angel Di Maria

Kocha Tito Vilanova.

 Barcelona: Valdes, Alves, Pique, Mascherano, Adriano, Busquets, Xavi, Iniesta, Alexis, Messi, Pedro.

Akiba: Fabregas, Puyol, Villa, Pinto, Jordi Alba, Sergi Roberto, Tello.



 Kocha  Jose Mourinho.

Real Madrid: Casillas, Arbeloa, Albiol, Sergio Ramos, Coentrao, Alonso, Khedira, Callejon, Ozil, Ronaldo, Benzema.

Akiba: Varane, Granero, Marcelo, Adan, Higuain, Di Maria, Lass Diarra, Nacho, Morata, Jesus.

 

Real Madrid coach Jose Mourinho believes that the linesman made a “big mistake” by allowing Pedro’s goal to stand during his side’s 3-2 defeat to Barcelona in the first leg of their Supercopa tie.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad