Nyoka mwenye umbo kama la viungo vya uzazi vya mwanaume wagunduliwa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, August 24, 2012

Nyoka mwenye umbo kama la viungo vya uzazi vya mwanaume wagunduliwa.


Nyoka mwenye umbo la Ajabu.
Wanasayansi nchini Brazil wamegundua aina ya nyoka vipofu wenye umbo kama uume wa binadamu.


Nyoka hawa wa ajabu aina ya ‘atretochoana eiselti’ walipatikana kwenye bwawa la kuzalisha umeme ambapo wakandarasi walikuwa wakifanya ukarabati kwenye misitu ya Amazon.



Wana baiolojia waliwapata nyoka hawa wenye umbo la ajabu sita wenye urefu wa mita moja chini ya mto Madeira huko Rondonia, Brazil.



Wanasayansi wamesema licha ya viumbe hao kuonekana kama nyoka lakini sio jamii ya reptilia.


Aidha Mara ya kwanza waligunduliwa America ya Kusini mwaka 1968.
 

Nyoka huyo anaweza akawa na muonekano usiopendeza katika jamii, lakini huu ni ugunduzi unaovutia kwa wanayasansi wanaomini kuwa wanauhusiano na vyura.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad