Wapanda pikipiki wanaofanya kazi ya kubeba abiria katika wilaya ya Ngara mkoani kagera wafanya kazi katika mazingira magumu. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, July 28, 2012

Wapanda pikipiki wanaofanya kazi ya kubeba abiria katika wilaya ya Ngara mkoani kagera wafanya kazi katika mazingira magumu.


Mkuu wa Wilaya ya Ngara Bw Constantine Kanyasu wa tatu kulia

Baadhi ya wapanda pikipiki wanaofanya kazi ya kubeba abiria katika wilaya ya Ngara mkoani kagera wamesema wanafanya kazi katika mazingira magumu kutokana na changamoto ya kukosa leseni kutoka makao makuu ya mkoa.


Wakizungumza katika mkutano na mkuu wa wilaya Bw Constantine Kanyasu, wapanda pikipiki hao wamesema kazi yao inakuwa ngumu kwa kukimbizana na polisi kutokana na kufanya kazi bila leseni.


Mwenyekiti wa wapanda pikipiki hao Bw Yazzidu Wilsoni amesema kwa sasa wamejiunga katika vikundi vya kukopeshana ili kupata fedha itakayowawezesha kupata mafunzo na leseni ambazo upatikanaji wake bado kero.

 
Hata hivyo Mkuu wa wilaya ya Ngara mkoani Kagera Bw Costantine Kanyasu ametoa muda wa miezi miwili kwa madereva wa vyombo vya usafiri wasio na leseni kuhakikisha wanazitafuta na kuzisajili ili kufanya kazi kwa kuzingatia sheria.


Bw Kanyasu amesema kwa kutumia umoja wao jeshi la polisi lifanye taratibu za kuwahamasisha watoa leseni mkoani kufika wilayani Ngara ili kutoa mafunzo Sambamba na leseni ili waweze kuendesha shughuli kwa kufuata sheria.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad