Mkazi wa Kariakoo jijini Dar es Salaam,anashikiliwa na jeshi la Polisi baada ya mita yake ya Luku kukutwa na yuniti za umeme elfu 29 na 365 zenye thamani ya shilingi milioni nane. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, July 28, 2012

Mkazi wa Kariakoo jijini Dar es Salaam,anashikiliwa na jeshi la Polisi baada ya mita yake ya Luku kukutwa na yuniti za umeme elfu 29 na 365 zenye thamani ya shilingi milioni nane.

Jingo la Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco)


Mkazi wa Kariakoo jijini Dar es Salaam, Ahmad Selemani anashikiliwa na jeshi la Polisi baada ya mita yake ya Luku kukutwa na yuniti za umeme elfu 29 na 365 zenye thamani ya shilingi milioni nane.


Meneja wa Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco) Kanda ya Ilala, Athanasius Nangali, amesema mtu huyo hajawahi kununua umeme tangu alipounganishiwa mita hiyo mwaka 2010.


Aidha katika tukio jingine lililotokea eneo la Kariakoo Mtaa wa Magila Meneja wa Hoteli ya Akubu Paradise, Inocent Masawe amekamatwa akiwa na yuniti elfu moja na mia moja za umeme kwenye mita yake ya Luku, zenye thamani ya shilingi milioni 4.


Bw Nangali amesema mteja huyo amekuwa akifanya ujanja wa kununua umeme kidogo kwa ajili ya matumuzi ya hoteli yake, lakini umeme uliomo kwenye mita ni mwingi kuliko kiasi anachonunua.


Kufuatia hatua hiyo ametoa wito kwa watanzania kutoa taarifa za wanaoihujumu TANESCO na kuahidi kuwa watuhumiwa wote waliokamatwa watafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad