Jiji la London yafungua michezo ya Olimpiki kwa shangwe huku Timu za Soka toka Nchi za Afrika zikianza kwa matokeo ya sare. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Saturday, July 28, 2012

Jiji la London yafungua michezo ya Olimpiki kwa shangwe huku Timu za Soka toka Nchi za Afrika zikianza kwa matokeo ya sare.


Inakadiriwa  Watu wapatao billioni 40 kote duniani waliangalia ufunguzi wa michezo ya Olimpiki katika televisheni.

Nchi ya Uingereza ilifungua michezo ya Olimpiki ya mwaka 2012 Ijumaa kwa mbwembwe za ndege za kivita zikipita juu ya uwanja, maonyesho ya fataki na halaiki iliyoonyesha historia ya michezo hiyo kuanzia 1896 mpaka sasa.

 

Karibu watazamaji 60,000 walishuhudia mwigizaji aliyevalia kama Malkia Elizabeth mwenye umri wa miaka 86 akiingia katika uwanja wa Olimpiki kwa parachuti akifuatana na mcheza sinema za James Bond - Daniel Craig. 

 

Muda mchache baadaye Malkia mwenyewe alisimama kimya wakati watoto wanaimba wimbo wa taifa "God Save the Queen".

 

Baadaye kidogo gwaride la mataifa lilifuatia huku wanamichezo zaidi ya 10,000 wakiingia uwanjani na kupita mbele ya jukwaa kuu huku Mataifa 204 yanashiriki katika michezo ya mwaka huu.


Mashindano hayo ya siku 17 katika michezo 26 yanaanza Jumamosi na kuendelea mpaka August 17.


Kila la kheri Timu ya Tanzania.

Aidha katika michezo iliyoanza Timu za Soka toka Nchi za Afrika zinazoshiriki Michezo ya OLIMPIKI LONDON 2012 zimecheza Mechi zake za mwanzo za Makundi na hakuna hata moja iliyoshinda isipokuwa sare kwa Timu za Gabon, Senegal na Morocco kwa Wanaume huku Misri ikifungwa bao 3-2 na Brazil na Timu za Wanawake zote zikifungwa.

 

Wanawake walicheza Mechi zao Jumatano July  25 mwaka huu na Banyana Banyana, Timu ya Afrika Kusini, ilipigwa bao 4-1 na Sweden na wenzao Cameroun walichapwa 5-0 na Brazil.


OLYMPIKI 2012  kutoka  LONDON, UINGEREZA ambapo


Matokeo kwa Wanaume  Alhamisi Julai 26

 

Honduras 2 Morocco 2

Gabon 1 Switzerland 1

Britain 1 Senegal 1

Brazil 3 Egypt 2

 

Matokeo kwa  wanawake  Julai 25

Cameroon 0 Brazil 5

Sweden 4 South Africa 1

 

Mechi  zifuatazo  ni Jumamosi  Julai 28 kwa Wanawake na Wanaume ni Jumapili Julai 29.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad