Shule ya msingi
Ruganzo.
|
Walimu
nchini Leo(July 30)mwaka huu wananza
mgomo kuitikia wito wa chama cha walimu nchini CWT ili kuishinikiza serikali
kuboresha maslahi yao.
Uchunguzi katika maeneo mbalimbali nchni umebaini kuwa
walimu wengi wameitikia wito wa kugoma kufanya kazi huku uchunguzi katika shule za msingi
Ruganzo, Ngara mjini ,Nakatunga na kumuyange wilayani Ngara mkoani Kagera umeonesha kuwa walimu wa shule
hizo hawakufika shuleni.
Mwalimu wa
shule ya Sekondari Ntobeye Bw Sharaza
Tadeo amesema hawezi kuingia darasani kwa kile alichokieleza kuwa serikali
imeshindwa kutatua kero zao.
![]() |
Katika
shule hizo walimu wakuu ndio walioonekana mashuleni huku wanafunzi
wakicheza michezo mbalimbali.
|
Wilayani
Kibondo mkoani Kigoma,Chama cha walimu CWT kimewataka wanachama
wake kuunga mkono mgomo ambapo Katibu wa
CWT wilayani humo Bw.Lazaro Nkwavu amesema mgomo huo utaendelea hadi hapo
Serikali itakapotekeleza madai yao.
Bw. Nkwavu
ameyataja baadhi ya madai yao kuwa ni pamoja na nyongeza ya mshahara kwa
asilimia 100,posho ya kufundishia 55% kwa walimu wa masomo ya Sayansi na
asilimia 50 kwa wanaofundisha masomo ya sana.
Katibu huyo
ameyataja madai mengine kuwa ni Posho ya kujikimu katika mazingira magumu,na
kuwataka walimu kutotishika kwa vitisho vinavyotolewa na baadhi ya maafisa wa
Serikali.
Katika hatua
nyingine jumla ya wabunge sita wametaka bunge lisitishe shughuli zake ili
lijadili mgomo wa walimuu ulioanza leo.
Wabunge hao
wakiongozwa na mbunge Yahya Kassim Issa wamelitaka bunge kusitisha shughuli
zake ili lijadili mgomo huo wa walimu nchi nzima.
Naibu Spika
wa Bunge Bw Job Ndugai amesema suala
hilo haliwezi kujadiliwa kwa kuwa limefikishwa mahakamani.
Bw Ndugai amesema taarifa alizopatiwa
zinaonyesha kuwa serikali pamoja na CWT wamewalisha hoja zao katika mahakama
kuu ambapo kesho (leo)july 31 ,mchana mahakama itaanza kusikiliza madai yao.
Sorce:radiokwizera.com
No comments:
Post a Comment