Timu
iliyopewa nafasi kubwa kwenye Michezo ya Olimpiki LONDON 2012, Hispania jana ilichapwa bao 1-0 na Honduras na kutupwa
nje ya Mashindano huku kwenye Makundi mengine Neymar akiibeba Brazil kutinga
Robo Fainali ikiambatana na Japan ambayo iliifunga Morocco 1-0 na Mkongwe Ryan Giggs alipachika bao moja
na kuisaidia Team GB kuichapa UAE bao 3-1.
Hispania wametolewa nje ya Olimpiki baada ya kupata
kipigo cha bao 1-0 mikononi mwa Honduras hiki kikiwa kipigo chao cha pili
kufuatia kufungwa 1-0 na Japan kwenye Mechi ya ufunguzi ya Kundi D.
Hispania wamebakisha
Mechi moja ya kukamilisha ratiba na Morocco.
Katika Mechi
nyingine ya Kundi D Japan wao wameingia Robo Fainali baada ya jana kuitungua
Morocco bao 1-0.
Nao Senegal
waliichapa Uruguay bao 2-0 kwenye Mechi ya Kundi A na kumaliza Mechi wakiwa Mtu
10 baada ya Mchezaji wao Abdoulaye Ba kutolewa kwa Kadi Nyekundu.
Katika Mechi
nyingine ya Kundi A, Wenyeji Team GB waliichapa United Arab Emirates bao 3-1
kwa bao za Ryan Giggs, Scott Sinclair na Daniel Sturridge.
Team GB sasa
inahitaji sare tu itakapocheza Mechi yake ya mwisho na Uruguay ili wasonge
mbele.
Nyota wa
Brazil, Neymar, aling’ara sana wakati Brazil ilipoichapa Belarus bao 3-1 katika
Mechi ya Kundi C na kuiwezesha Brazil kutinga Robo Fainali.
Neymar
alifunga bao la pili kwa frikiki na bao nyingine mbili zilizofungwa na
Alexandro Pato na Oscar zilitengenezwa nae.
Belarus ndio
waliotangulia kupata bao katika Dakika ya 8 mfungaji akiwa Renan ambae ni mzaliwa
wa Brazil.
Kwenye Mechi
nyingine ya Kundi C, Egypt na New Zealand zilitoka sare bao 1-1.
Katka Mechi
ya Kundi B, Mexico waliichapa Gabon bao 2-0 kwa bao za Dos Santos.
Aidha
mashindano hayo yakiwa yanaendelea,China na Marekani wanaongoza kwa MEDALI huku
Africa ya Kusini ikishinda Medali kwa Africa.
| | | |||
---|---|---|---|---|---|
Rank | Country | Gold | Silver | Bronze | |
1 | 9 | 5 | 3 | 17 | |
2 | 5 | 7 | 5 | 17 | |
3 | 3 | 1 | 3 | 7 | |
4 | 3 | 0 | 1 | 4 | |
5 | 2 | 4 | 2 | 8 | |
6 | 2 | 2 | 2 | 6 | |
7 | 2 | 0 | 3 | 5 | |
8 | 2 | 0 | 0 | 2 | |
9 | 1 | 4 | 6 | 11 | |
10 | 1 | 2 | 1 | 4 | |
11 | 1 | 2 | 0 | 3 | |
12 | 1 | 1 | 1 | 3 | |
12 | 1 | 1 | 1 | 3 | |
14 | 1 | 1 | 0 | 2 | |
15 | 1 | 0 | 2 | 3 | |
16 | 1 | 0 | 0 | 1 | |
16 | 1 | 0 | 0 | 1 | |
16 | 1 | 0 | 0 | 1 | |
19 | 0 | 2 | 0 | 2 | |
20 | 0 | 1 | 2 | 3 | |
21 | 0 | 1 | 0 | 1 | |
21 | 0 | 1 | 0 | 1 | |
21 | 0 | 1 | 0 | 1 | |
21 | 0 | 1 | 0 | 1 | |
21 | 0 | 1 | 0 | 1 | |
21 | 0 | 1 | 0 | 1 | |
27 | 0 | 0 | 1 | 1 | |
27 | 0 | 0 | 1 | 1 | |
27 | 0 | 0 | 1 | 1 | |
27 | 0 | 0 | 1 | 1 | |
27 | 0 | 0 | 1 | 1 | |
27 | 0 | 0 | 1 | 1 | |
27 | 0 | 0 | 1 | 1 | |
27 | 0 | 0 | 1 | 1 | |
27 | 0 | 0 | 1 | 1 | |
27 | 0 | 0 | 1 | 1 | |
27 | 0 | 0 | 1 | 1 |
No comments:
Post a Comment