Askofu wa Kanisa
Katoriki jimbo la Rulenge Ngara Askofu Severin
Niwemugizi amezindua Kanisa la Mtakatifu Paulo Kigango cha Kasuno Parokia
ya Katoke lililogharimu zaidi ya shilingi milioni 12 mpaka kukamilika kwake.
Shughuli hiyo ya uzinduzi imefanyika hapo May 25, 2018 kijijini Kasuno ambapo Baba Askofu anaendelea na ziara yake ya ukaguzi mbali mbali wa shughuli za maendeleo katika parokia ya katoke shughuli ambazo zinaenda sambamba na uwekaji wa jiwe la msingi pamoja na uzinduzi wa makanisa mbali mbali.
Mhashamu Askofu
Severin Niwemugizi amewapongeza
waumini wa kanisa la mtakatifu Paulo Kasuno kwa kushiriki pamoja kwa umoja na
kuweza kujenga kanisa zuri kwani ni hatua kubwa ukilinganisha na kanisa la
lililojengwa kwa nyasi walilokuwa wakitumia zamani.
Awali Katibu
wa Kigango cha Kasuno Bw. Rucas Raulent
akisoma lisara mbele ya baba askofu amesema kuwa ujenzi wa kanisa hilo
lililogharimu zaidi ya milioni 12 umetokana na michango ya waumini wa kanisa
hilo waliojitolea pia nguvu kazi kama kusomba mawe,kokoto na matofari.
kwa upande
wao waumini wa Kanisa Katoriki la Mtakatifu Paulo Kigango cha Kasuno
wamepongeza ujio wa Baba Askofu na kwamba ujio huo utaongeza hamasa kwa waumini
hata ambao walikuwa wamekuwa wapagani.
Na James Jovin -Radio Kwizera Biharamulo.
Na James Jovin -Radio Kwizera Biharamulo.
No comments:
Post a Comment