Mkuu wa Mkoa
wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu (kushoto) akipokea Msaada kutoka kwa
Meneja wa Kanda ya Ziwa Bw. Abraham
Augustine (kulia) uliotolewa na Benki ya NMB Mkoani Kagera katika Zahanati
ya Nyanga Manispaa ya Bukoba leo May 25, 2018.
Na: Sylvester
Raphael-Kagera.
Benki ya NMB
Mkoani Kagera yatoa misaada ya Shilingi Milioni 20,000,000/= ya Vifaa
Tiba na Samani kwa ajili ya Shule za Msingi na Sekondari katika Halmashauri ya
Wilaya ya Bukoba na Manispaa ya Bukoba ili kuboresha huduma za Jamii katika
Halmashauri hizo.
Misaada hiyo
imetolewa mapema leo Mei 25, 2018 katika Zahanati ya Nyanga Manispaa ya Bukoba
ambapo katika Zahanati hiyo Benki ya NMB Mkoa wa Kagera ilitoa Vitanda 6,
Magodaro 6, Vitanda viwili vya kujifungulia Wajawazito na Boksi moja la vifaa
vya vinavyotumika wakati wa kujifungua akinamama, vifaa tiba hivyo vikiwa na
thamani ya shilingi milioni 5,000,000/=.
Aidha, Benki
hiyo ilitoa Madawati 100 yenye thamani ya shilingi milioni 10,000,000/= katika
shule za Msingi Kyaitoke na Kitwe kila shule madawati 50. Pia Shule ya
Sekondari Bukara ilipokea viti 60 na meza 60 vyenye thamani ya shilingi milioni
5,000,000/= kutoka katika Benki hiyo na kukamilisha jumla ya shilingi milioni
20,000,000/=.
|
Akikabidhi
misaada hiyo kwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meneja wa Kanda ya Ziwa Bw. Abraham Augustine alisema kuwa
Benki ya NMB imeamua makusudi kujikita katika kuhudumia jamii hasa katika Sekta
za Elimu na Afya ili kuigusa jamii ya Watanzania moja kwa moja.
Bw. Augustine aliongeza kuwa katika mwaka huu 2018
Benki hiyo imetenga shilingi Bilioni 1 kwaajili ya kuihudumia jamii na tayari
misaada mbalimbali imeishatolewa katika Sekta za Elimu na Afya yenye thamani ya
shilingi Milioni 100 na mkoa wa Kagera tayari umenufanika.
Bw. Augustine alimalizia kwa kusema kuwa Benk ya
NMB inarudisha faida inayoipata kwa wananchi kutokana na biashara wanayoifanya
ili kuhakikisha kila mwananchi ananufaika na faida hiyo hasa kupitia huduma za
kijamii katika Sekta za Elimu na Afya.
|
Mara baada
ya kupokea misaada hiyo Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu aliishukura sana Benki ya NMB kwa
kurudisha faida kwa wananchi kupitia kutoa misaada ya kuboresha huduma za jamii
kama Afya na Elimu
Mhe. Kijuu alitoa wito kwa Taasisi na Mashirika
mbalimbali ya Serikali na yasiyokuwa ya Seriakli hasa Taasisi za Kibenki
kuiga mfano mzuri wa Benki ya NMB kwa kuiunga mkono Serikali katika
juhudi zake za kuboresha miundombinu ya kutolea huduma za kijamii kama shule na
Sekta ya Afya ili wananchi wapate huduma bora.
Mkuu a Mkoa
Kijuu alitolea mfano Sekta ya Elimu kuwa baada ya Serikali kutoa Sera ya Elimu
bila malipo kumekuwa na mwitikio mkubwa wa wazazi kuwaandikisha wanafunzi kwa
wingi katika shule jambo ambalo linaifanya miundombinu iliyokuwepo hapo awali
kuonekana kuwa ni michache kwahiyo Serikali kwa kishirikiana na wananchi na
wadau wengine wote wanatakiwa kuiboresha miundombinu hiyo ili kukidhi uhuhitaji
ili huduma bora itolewe.
|
Picha ya Pamoja.
Aidha, Mara
baada ya kupokea msaada wa meza na viti meza kwaniaba ya Halmashauri ya Wilaya
ya Bukoba Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mhe. Kashasha aliishukuru benki
ya NMB na kusema kwamba msaada huo umewafikia kwa wakati muafaka ulipokuwa
unahitajika.
Naye Mhe.
Jimmy Kalugendo Naibu Meya wa Manispaa ya Bukoba alisema kuwa Vifaa Tiba
vilivyotolewa na Benki ya NMB Katika zahanati ya Nyanga ni msaada mkubwa katika
kituo hicho kwani vifa atiba hivyo vilikuwa vimekwamisha Zahanati kufunguliwa
lakini sasa itafunguliwa na kuanza kutoa huduma bora kwa wananchi wa eneo hilo.
|
Mkoa wa Kagera unayo matawi 22 ya Benki ya NMB na tawi la mwisho kufunguliwa ni Tawi la Kabanga Wilayani Ngara na kuna uwezekano wa Tawi lingine kufunguliwa Kamachumu Wilayani Muleba ili kutoa huduma kwa wananchi wa Nshamba, Rubya na Kamachumu . |
No comments:
Post a Comment