![]() |
Azam FC.
Nacho Kikosi
cha Klabu Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, kimefanikiwa kuchomoza
na ushindi mnono wa mabao 5-0 dhidi ya timu ya Shupavu FC mchezo uliyopigwa Mkoani
Morogoro.
Waliyokuwa
mashujaa katika mchezo huo ni Azam FC ni Yahya Zayd aliyeanza kuiandikia
bao la kwanza timu hiyo, Idd Kipwagile na Paul Peter aliyehitimisha karamu ya
magoli kwa kupiga hat trick.
|
![]() |
Azam FC
imeingia kwenye mchezo huo dhidi ya timu hiyo inayoshiriki Ligi Daraja la Pili
Tanzania Bara (SDL) ikiwa na kumbukumbu ya kuitoa Area C United ya Dodoma kwa
mabao 4-0, yaliyofungwa na kiungo Salmin Hoza, Nahodha Msaidizi Agrey Moris,
Yahya Zayd na Enock Atta.
Michuano
hiyo ya Azam Sports Federation Cup ina umuhimu mkubwa kwa kila timu
inayoshiriki kwakuwa mshindi huiwakilisha nchi katika Kombe la Shirikisho Barani
Afrika.
|
No comments:
Post a Comment