IGP Sirro.-Wananchi Tupeni Ushirikiano katika kuwafichua Wahalifu Nchini. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Friday, September 08, 2017

IGP Sirro.-Wananchi Tupeni Ushirikiano katika kuwafichua Wahalifu Nchini.

IGP Sirro.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Nyakoro Sirro leo Septemba 8, 2017 amezungumza na waandishi wa habari na kueleza kuhusu matukio ya uvunjifu wa amani yanayoendelea hapa nchini.

Sirro amezungumzia juu ya mauaji ya Kibiti na kusema hali sasa ni tulivu na asilimia 90 ya wahalifu wameshakamatwa.

 Pia amezungumzia juu ya kauli ya jana ya Rais Magufuli kuhusu kuwakamata waliotajwa kwa kashfa ya madini kwenye ripoti ya Biashara ya Tanzanite na Almasi na kusema kuna watu wameshakamatwa mkoani Manyara tayari huku akieleza kuwa tukio la watoto kutekwa Arusha kwa sasa watuhumiwa wameshakamatwa na mmoja wao ameshauawa huku upelelezi ukiendelea.

Akizungumzia suala la Tundu Lissu kupigwa risasi amesema wametuma wapelelezi wao wazuri kwenda Dodoma na lazima watawakamata, akaongeza kuwa itawezekana kama wananchi watawapa taarifa.


No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad